Na Khadija Seif,Globu ya jamii
KIJANA
Khamis Salum mwenye ulemavu wa miguu awapongeza wasanii wa Bongomovie
kwa kumtembelea na kumpatia baadhi ya mahitaji nyumbani kwake Yombo
jijini Dar es salaam.
Akizungumza
na waandishi wa habari Salum amesema ni faraja kubwa ameipata na
hakutegemea kama wasanii wangeweza kumkumbuka na kumpelekea baadhi ya
mahitaji kama vile mchele,magodoro pamoja na fedha.
Hata
hivyo ameomba apatiwe msaada wa kitabibu kutokana na maumivu makali
anayoyapata siku hadi siku na kumsababishia kushindwa kutimiza ndoto
zake kama kijana .
"Naamini
nitaweza kusimama tena naomba Rais wetu wa wanyonge Dk.John Magufuli
pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda wasikie kilio
changu kwani nateseka sana, ukizingatia mimi kiumri bado mdogo nahitaji
kusoma na kutimiza malengo yangu," amesema Salum.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Nitete Frola Rauo amesema Salum
anahitaji kupendwa,kuthaminiwa na kutunzwa na watu wote kwani ni kijana
mdogo sana na anahitaji msaada wa hali na mali.
Rauo
amesema kupitia shirika la Nitetee ambalo lipo kwa ajili ya kusaidia
watu waliweza kufanya mikakati ya kuhakikisha wanamtoa Salum pale
Kariakoo na kumtafutia sehemu ya kuishi ambayo ni yombo kwa sasa
"Tulimpeleka
hospital kwa ajili ya vipimo mbalimbali na kugundua tatizo lake la
miguu kuvimba linazidi kukua siku hadi siku tofauti na hapo awali,"
amesema Rauo
Hata
hivyo kiongozi wa Msafara huo ambae ni Msanii wa Bongomovie Steven
Mengere a.k.a Stive Nyerere amesema Salum ni watoto kama watoto wengine
wanahitaji kutazamwa kwa jicho la kipekee kwa sasa kutokana na maradhi
yanayomsumbua ya miguu kuwa mikubwa na kumlazimu kukaa ndani na kuwa
tegemezi kwa kila kitu.
"Sisi
wasanii tujitathimini na kulichukua jukumu la kumsaidia mtoto huyo kwa
sasa na kuwahamasisha jamii inayotuzunguka na taifa kwa ujumla
kuhakikisha Khamis anasimama," amesema Steve Nyerere.
Pia
ameeleza kuwa mahitaji madogo waliyompatia hayataishia hapo bali
watarudi kujipanga upya na kuhakikisha wanampatia vitu vingine ikiwemo
kumlipia chumba,fedha pamoja na vingine.
Kijana
mwenye tatizo la miguu kujaa Khamis salum akizungumza na waandishi wa
habari pamoja na wasanii baada ya kumtembelea anapoishi kwa sasa yombo
jijini Dar es salaam.
Msanii
wa Bongomovie Steven Nyerere akizungumza na waandishi wa habari pamoja
na wasanii waliofika kumtembelea mtoto Khamis salum na kuwasilisha
mahitaji yake salum jijini Dar es salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...