Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas,ameongoza kikosi maalum katika kupambana na uhalifu nchini kilichoungana na vikosi  vya jeshi la Polisi mkoa wa Njombe katika kufanya Operesheni katika mapori ya  Nundu na Tanwat mkoani Njombe kuwasaka watuhumiwa wa Mauaji ya watoto. Picha na jeshi la Polisi     


 Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas, pamoja na Kamanda wa Polisi Mkoa Njombe Kamishina Msaidizi Mwandamizi SACP Afande  Renata Mzinga  wameongoza kikosi maalum cha  kupambana na uhalifu nchini kilichoungana na vikosi  vya Jeshi la Polisi mkoa wa Njombe katika kufanya Operesheni katika mapori ya  Nundu na Tanwat mkoani Njombe.(Picha na jeshi la Polisi) 




Jeshi la Polisi Makao Makuu Kitengo Maalum cha Kupambana na uhalifu kikiongozwa na Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Naibu Kamishna Liberatus Sabas, kimeshirikina na Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe kuendesha Operesheni Maalum ya kukabiliana na matukio ya mauaji ya watoto wadogo ambayo yamejitokeza mkoani humo, mpaka sasa watuhumiwa 30 wamekamatwa waliojihusisha na matukio hayo, 

Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Naibu Kamishna Liberatus Sabas, amesema watuhumiwa hao ifikapo Jumatatu watakuwa wamefikishwa Mahakamani kukabiliana na tuhuma za mauaji ya watoto, Aidha Naibu Kamishna Sabas, amewataka watanzania kutoa Taarifa za wahalifu popote walipo na amewahakikishia watanzania kuwa matukio hayo yamekoma sasa 

Aidha Naibu kamishna Sabas amesema Jeshi La Polisi halitamuonea mtu yoyote haya awe Mfanyabishara, Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Dini, au Waganga wa Kienyeji watakaojihusisha na matukio ya mauaji kwa njia yoyote ile sheria itachukua mkondo wake huku akiapa kupambana na wahalifu wa mauaji yoyote yale kindakindaki

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...