Kocha Mkuu wa timu ya KMC ya Manispaa ya Kinondoni, Etiene Ndayiragije akiwa pamoja na Mchezaji wa timu ya Alliance FC yenye maskani yake jijini Mwanza Tanzania, Dickson Ambundo.
Kocha Mkuu wa timu ya KMC ya Manispaa ya Kinondoni, Etiene Ndayiragije, akionyesha furaha baada kupokea tuzo ya Bikosports Tanzania, kufuatia kuwa kocha kocha bora wa mwezi Januari, ambapo Kampuni ya BikoSports waendeshaji wa mchezo wa kubashiri matokeo ya michezo mbalimbali duniani ndio wadhamini wa tuzo hiyo waliobarikiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Picha na Mpigapicha Wetu.
Mchezaji wa timu ya Alliance FC yenye maskani yake jijini Mwanza Tanzania, Dickson Ambundo, akiwa mwenye shangwe nyingi baada ya kupokea tuzo ya mchezaji bora wa mwezi January kutoka kwa Msemaji wa Bikosports, Geofrey Lea, waendeshaji wa mchezo wa kubashiri matokeo ya michezo mbalimbali duniani ambao ndio wadhamini wa tuzo hiyo waliobarikiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

WAENDESHAJI wa mchezo wa kubashiri matokeo wa Bikosports, jana wamewakabidhi tuzo zao,  Etiene Ndayiragije, Kocha Mkuu wa timu ya KMC ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na mchezaji wa Alliance FC ya jijini Mwanza, Dickson Ambundo, baada ya kuibuka kocha bora na mchezaji bora wa mwezi January.

Makabidhiano ya tuzo hizo yalifanyika Makao Makuu ya Bikosports jijini Dar es Salaam, huku tuzo hizo zikiwa na lengo mahususi la kuongeza ari katika harakati za kukuza na kuendesha mpira wa miguu nchini Tanzania.

Akizungumzia tuzo hiyo, Kocha wa KMC, Etiene Ndayiragije, aliwashukuru Bikosports kwa kuamua kuingia kwenye tuzo hizo akiamini kuwa kwa pamoja zitafanikisha sekta ya mpira wa miguu kupiga hatua kubwa.

"Nawashukuru walioniona kwamba nastahili kuwa kocha bora wa mwezi January, huku tuzo hii nikiamini nimeipata kwa sababu ya sapoti kubwa ninayoipata kutoka kwa wachezaji wangu wote pamja na uongozi wangu wa KMC," Alisema Ndayiragije.

Naye Ambundo aliyeibuka kwenye Mchezaji Bora wa mwezi January, alisema kwa kupata tuzo ya Bikosports anaamini ataongeza bidii kubwa katika safari yake ya mpira wa miguu, jambo ambalo limechangiwa na nguvu kubwa anayoiweka katika timu yao ya Alliance yenye ndoto kubwa ya kufanya vizuri.

"Nadhani nimestahili kabisa kuitwaa tuzo hii na ninaamini kuwa naweza kuipata tena kwa sababu lengo langu ni kucheza mpira mzuri na kuisaidia timu yangu ya Alliance, hivyo ninachofanya ni kuongeza nguvu katika kumsikiliza mwalimu wangu, kuishi vizuri na wachezaji wenzangu ili wote tufikie malengo yetu," Alisema Ambundo.

Akizungumzia tuzo hiyo, Msemaji wa Bikosports, Geofrey Lea alisema kuanzisha tuzo hiyo ni sehemu ya kuhakikisha kwamba mpira unakuwa kwa kiasi kikubwa, huku wakiomba ushirikiano mkubwa kutoka kwa wadau wa mpira wa miguu wakiwamo wanaobashiri matokeo kwa kupitia kampuni yao ya Bikosports.
"Hii ni safari nzuri ya kukuza mpira wa miguu hivyo wadau wote kwa pamoja tunaomba ushirikiano wao, ambapo katika nyanja ya ubashiri wa matokeo, 

Bikosports ndio Kampuni inayotoa zawadi kwa haraka huku jamvi lao likiwa ni rahisi kushinda kuliko michezo yoyote Tanzania, ambapo namba ya Kampuni ni 101010, huku mchezaji akiweza kubashiri kwa simu ndogo kwa namba *149*89# au wanaobashiri kwa mtandao https://www.bikosports.co.tz/ ambao ni rahisi kucheza na kushinda pia," Alisema Jeff Lea.

Kuanzishwa kwa tuzo ya Bikosports kwa kocha bora na mchezaji bora ni sehemu muhimu ya kuhakikisha kwamba wachezaji na makocha wao wanaongeza bidii kubwa katika kuhakikisha kwamba wanapata maendeleo makubwa ndani ya uwanja, ambapo mbali na tuzo hizo, pia huambatana na Sh Milioni moja.
mwisho

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...