Mwanamke huyu alikuwa tayari amefika katika kituo cha kupiga kura.

Hatua ya kuahirishwa kwa uchaguzi wa urais na ubunge nchini Nigeria saa tano kabla ya zoezi la upigaji imezua mjadala mkali kote nchini humo.

Baadhi ya watu ambao hawakua na habari uchaguzi umeahirishwa walikuwa wamefika klatika vituo vyao vya kupigia kura.

Musa Abubakar, ambaye alisafiri umbali wa kilomita 550 (340 miles) kutoka mji mkuu wa Abuja ili kupiga kura katika mji wa kaskazini wa Daura, ameiambia BBC "haamini" kilichotokea.

Yeye ni mmoja wa raia wengi wa Nigeria waliyosafiri kutoka mji mmoja hadi mwingine kushiriki zoezi la upigaji kura.

"Sijui la kufanya. Sijafurahia hatua hii hata kidogo," alisema bw Abubakar.

Sasa anakabiliwa na kibarua cha kuamua ikiwa atasubiri kupiga kura Daura kisha arudi kazini Abuja ama ajiandae kwa safari ya pili au kuachana kabisa na shughuli hiyo

Baadhi ya watu waliamua kuangazia hasira zao katika mtando wa kijamii wa Twitter, kwa kutumia Hashtag ya "waahirishwa", "kuahirishwa" na "Inec".

Bobby Ezidi, alisema tume ya uchaguzi imezembea katika kazi yake .Wengine wamekuwa wakisambaza kanda ya video inayomuonesha bw Yakubu akisisitiza kuwa kila kitu kiko shwari "uchaguzi hautaahirishwai" na kujiuliza nini kilichobadilika.

Tume huru ya kitaifa ya uchaguzi (INEC) ilitangaza hatua hiyo saa tano tu kabla ya wapiga kura kuelekea katika vituo vya upigaji kura hii leo Jumamosi.

"Haiwezekani kuendelea na zoezi la uchaguzi kama ilivyopangwa," mwenyekiti wa tume hiyo Mahmood Yakubu amesema, akitaja hitilafu za kimipango.

Amesema uamuzi huo mgumu umehitajika kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa huru na haki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...