Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema vituo vya afya 350 vitakuwa vimekamilika nchi nzima ndani ya miaka mitano ya Uongozi wa Awamu ya tano
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati alipotembelea kituo cha afya cha Sokoine wilayani ya Singida mkoa wa Singida ikiwa muendelezo wa ziara yake ya kikazi ambapo amekuwa akikagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo.
“Kulikuwa na hospitali 65 za wilaya lakini tulivyoingia madarakani zimejengwa hospitali 67 na lengo kuu ni kuwapa wananchi huduma bora ya afya” alisema Makamu wa Rais.
Aidha Makamu wa Rais alisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano haitokubalina na misaada ya masharti na imejidhatiti kufanya miradi ya maendeleo kwa kutumia fedha zake za ndani.
Pamoja na mambo mengine Makamu wa Rais alizindua barabara ya Karume ambayo inajumuisha mradi wa mtandao wa barabara wenye urefu wa kilomita 6.1 ambazo nibarabara ya Karume yenyewe , Boma Kinyeto, Double Road Junction (Semali Singida-Dodoma ).
Sambamba na hayo, Mheshimiwa Makamu wa Rais alitembelea kituo cha afya Migori ambapo alijionea maendeleo ya ujenzi ambao unatazamiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi machi, pia alitembelea shule ya sekondari ya Mwanamema Shein ambapo alizungumza na wanafunzi na kujionea maendeleo ya ujenzi wa bweni la wanafunzi pamoja na kupanda mti wa kumbukumbu.
Wakati huo huo Naibu Waziri wa maji ameahidi kutoa tanki la maji la lita 10,000 kwa ajili ya kituo cha afya cha Karume ikiwa kama jitihada za kumuunga mkono Makamu wa Rais ambaye amejitoa kuhakikisha afya ya mama na mtoto inakuwa salama.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya Migori wilayani
Singida kutoka kwa Kaimu Mhandisi wa Wilaya Dayness Rwehumbiza. Kituo
cha afya cha Migori ni moja ya vituo vilivyopata shilingi milioni 400 za
kitanzania. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akisalimia na Mkuu wa Sule ya Sekondari ya Mwanamema Shein Bi. Zainab
Mtindu wakati akiwasili kwenye shule hiyo iliyopo Migori, wilayani
Singida. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Wanafunzi
wa Shule ya Sekondari ya Mwanamema Shein iliyopo Migori wilayani
Singida wakiimba wimbo maalum wa kumkaribisha Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye yupo ziarani
mkoani Singida. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Naibu
Waziri wa Maji Mhe. Juma Awesu akizungumza na wanafunzi wa shule ya
sekondari ya Mwanamema Shein iliyopo Migori, Singida ambapo aliwasihi
wasome kwa bidii ili waje kuwa viongozi bora.(Picha na Ofisi ya Makamu
wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akiweka udongo kwenye mti wa kumbukumbu alioupanda katika shule
ya sekondari ya Mwanamema Shein iliyopo Migori wilayani Singida. (Picha
na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Naibu Waziri Ujenzi Mhe. Elias Kwandikwa akizungumza wakati wa hafla
fupi ya kuweka jiwe la msingi wa ufunguzi wa barbara ya Karume iliyopo
Singida mjini ambapo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ndio alikuwa
mgeni rasmi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuweka jiwe la msingi wa ufunguzi wa
barbara ya Karume iliyopo Singida mjini. (Picha na Ofisi ya Makamu wa
Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan akiweka jiwe la msingi kwenye ufunguzi wa barabara ya Karume
iliyopo Singida mjini. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...