Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia akiwasili wakati wa hafla ya utoaji Tuzo ya Kiswahili ya Mabati –Cornell ya Fasihi ya Afrika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia akihutubia wakati wa hafla ya utoaji Tuzo ya Kiswahili ya Mabati –Cornell ya Fasihi ya Afrika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia akimkabidhi cheti cha ushindi wa tuzo ya Fasihi Bw. Jacob Ngumbau Julius wakati wa hafla ya utoaji Tuzo ya Kiswahili ya Mabati –Cornell ya Fasihi ya Afrika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia akimkabidhi   tuzo ya ushindi katika Fasihi Bi. Zainab Alwi Baharoon wakati wa hafla ya utoaji Tuzo ya Kiswahili ya Mabati –Cornell ya Fasihi ya Afrika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wamiliki wa viwanda kurudisha fadhila kwa jamii ikiwemo kuwekeza katika lugha ya Kiswahili.

Makamu wa Rais ameyasema hayo leo kwenye hafla ya utoaji wa Tuzo ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasiji ya Kiafrika iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

“kwa hakika hii lugha haiwezi kupiga hatua bila kuwekewa uwekezaji wa dhati utakaojumuisha Serikali, sekta binafsi na asasi za kiraia”alisema Makamu wa Rais. Makamu wa Rais alisisitiza kuwa maendeleo yeyote ya Taifa hayawezi kufikiwa bila kuwa na lugha ya mawasiliano inayounganisha watu wa ndani ya nchi na hata nje ya nchi.

Tuzo hizi zimedhaminiwa na kampuni ya kutengeneza mabati ya ALAF Limited Tanzania pamoja na mshirikika wake kampuni ya Mabati Rolling Mills,Kenya kwa ushirikiano wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Aidha, Serikali imeendelea kuwatafutia walimu wetu wa Kiswahili fursa mbalimbali za ajira ikiwemo kuwapeleka nchi jirani pamoja na kuzishawishi nchi hizi kukifanya Kiswahili kuwa lugha rasmi. 

Makamu wa Rais ametoa rai kwa waandaaji kuangalia namna ya kuhamasisha washiriki kutoka nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika.Makamu wa Rais alionyesha umahiri wake pale alipoamua kughani moja ya beti kutoka kwa mshahiri maarufu mkongwe Mzee Haji Gora.

Pamoja na mambo mengine Makamu wa Rais alisisitiza jamii kuienzi lugha ya Kiswahili kwani imekuwa kiungo muhimu baina ya familia na koo mbali mbali hapa nchini.Kwa upande wake Waziri wa Viwanda na Uwekezaji alisema matumizi ya lugha rahisi yanachagia kukuwa kwa maarifa na uelewa mahala pa kazi.

Washindi wa tuzo ya Kiswahili mwaka huu ni Bi. Zainab Alwi Baharoon na Bw. Jacob Ngumbau Julius.Wakati huohuo Makamu wa Rais alizindua kitabu cha washindi wa mwaka 2017, Bw. Ally Hilal na Doto Rangimoto .

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Viongozi mbali mbali na wadau wa Kiswahili kutoka sehemu mbali mbali duniani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...