Aliwapika na kuwajenga mwenyewe kwa mambo mengi na mwisho alikiri  wazi kuwa sasa vijana hawa wameiva,Ruge hakuwaacha hivi hivi aliwapa zawadi ama cheti cha shukurani,kama ambayo anaonekana pichani akimkabidhi msanii wa bongofleva Mwasiti Almasi cheti cha kuhitimu mafunzo ya muziki katika kituo cha nyumba ya vipaji THT
Ruge hakuwaacha vijana wake hivi hivi ,aliwapa zawadi ama cheti cha shukurani,kama ambayo anaonekana pichani akiwakabidhi baadhi ya wasanii wa bongofleva cheti cha kuhitimu mafunzo ya muziki katika kituo cha nyumba ya vipaji THT




Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishali wa Clouds Media Group Ruge Mutahaba akizungumza jambo kwenye moja ya hafla za kampuni hiyo akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Joseph Kussaga,huku wakiwa wamezungukwa na baadhi ya wafanyakazi
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Joseph Kussaga akiungumza jambo huku Ruge Mutahaba akisikiliza kwa makini,kweye moja ya hafla za kampuni hiyo.
Ruge Mutahaba,mara nyingi hakupenda makuu,aliwaacha vijana aliowafungulia Dunia kuonesha umahiri wao katika mambo mbalimbali na yeye kukaa pembeni yao huku akiwatazama na kuwasikiliza,kama ambavyo anaonekana kwenye picha hizi.
Ruge Mutahaba alianzisha jukwaa la Fursa la kuwawezesha vijana katika mambo mbalimbali,pamoja na kuwa mwanzilishi kuna wakati aliamka na kutoa neno kama anavyoonekana pichani
Ruge Mutahaba akimuongoza aliyekuwa Waziri Mkuu awamu ya nne,Mh Fredrick Sumaye alipokwenda kutembelea kampuni hiyo ya Clouds Media Group na kuoneshwa mambo mbalimbali yaliyokuwa yakifanywa na kampuni hiyo.
Ruge akiwa na mgeni wake Mh Sumaye  ndani ya Studio za Clouds FM akimfafanulia jambo hatua kwa hatua.
Ruge Mutahaba pia hakuwa mkimya muda wote,wakati mwingine alijichangana na sehemu za watoto kama hivi na kutoa maono yake kwa jambo husika ikiwemo na kushauri nini kifanyike kusoga mbele zaidi 
Vijana wengi walipenda kumsikiliza Ruge,hasa kwa lugha alizokuwa akitumia nyepesi na zenye kutia hamasa ya kusikiliza zaidi kama anavyoonekana pichani

Ruge hakuacha kuwaelekeza ama kuwakumbusha jambo vijana wake wakati wowote na mahali popote pindi akutanapo,pichani alikuwa akizungumza jambo na mmoja wa watangazaji wa Clouds FM Hamis Mandi almaarufu kwa jina la Bdozen
Ruge Mutahaba akionekana na baadhi ya wasanii wa bongofleva walipokwenda kumjulia hali Mzee Njenje nyumbani kwake Sahare mkoani Tanga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...