Na Ripota Wetu  
JESHI la Polisi nchini Indonesia limeomba msamaha kwa kutumia nyoka kumtishia mtuhumiwa wa wizi baada ya video kusambazwa katika mitandao ya kijamii nchini humo. Baadhi ya maofisa wa jeshi hilo la polisi katika video hiyo wameonekana wakicheka na wengine waliokuwa wakimhoji mtuhumiwa huyo wakionekana kumuweka nyoka shingoni mwa mshukiwa huyo aliyekuwa amefungwa pingu huku akipiga kelele mashariki mwa eneo la Papua.

Habari iliyowekwa kwenye Mtandao wa Shirika la Habari la Uingereza(BBC) inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alifikishwa polisi kutokana na tuhuma za kuiba simu ya mkononi. Akizungumzia tukio hilo, Ofisa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini humo Tonny Ananda Swadaya amesema haikupaswa kufanyika hivyo lakini ametetea mbinu hiyo akieleza kwamba nyoka huyo hana sumu na kwamba wamechukua hatua kali dhidi ya maofisa waliohusika.

Swadaya amefafanua kuwa maofisa hao wa polisi hawakumpiga mshukiwa na kuongeza walichukua hatua kwa hiari yao kujaribu kumfanya mshukiwa akiri makosa. Kwa upande wake Wakili anayetetea haki za binaadamu Veronica Koman ametuma ujumbe kwenye mtandao wa Twitter ulioonyesha video hiyo, akidai kuwa maofisa hivi karibuni walimtishia mwanaharakati anayetetea uhuru wa Papua kwa nyoka akiwa gerezani.

Hata hivyo inaelezwa sauti katika video hiyo iliyosambaa inaarifiwa kusikika ikitishia kumweka nyoka huyo ndani ya mdomo wa mshukiwa na ndani ya suruali yake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...