RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dkt. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mkurugenzi Kinga Wizara ya Afya Zanzibar Dkt. Fadhil Mohammed, baada ya kuweka jiwe la Msingi Kituo hicho cha Afya kilichojengwa na Mradi wa Tasaf na Nguvu za Wananchi wa Shehia ya Kianga,wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Magharibi A Unguja leo.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mkurugenzi Kinga Wizara ya Afya Zanzibar Dkt. Fadhil Mohammed, (katikati) anayefuata ni Daktari Dhamana Wilaya ya Magharibi A Unguja. Dkt.Amina Hussein, na wa mwisho Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ  Haji Omar Kheri.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, akipanda mti wa muembe katika eneo la Kituo cha Afya Kianga Wilaya ya Magharibi A Unguja baada ya kuweka jiwe la msingi leo, akiwa katika ziara yake katika Wilaya hiyo.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi Kituo cha Afya Kianga, Wilaya ya Magharibi A Unguja, akiendelea na ziara yake kutembelea Miradi ya Maendeleo.
 MKURUGENZI Mkuu wa TASAF Tanzania Ndg. Ladislous Mwamanga, akizungumza na kutoa salamu za Tasaf wakati wa Uwekaji wa Jiwe la Msingi Kituo cha Afya katika Kijiji cha Kianga kilichojengwa na Mradi wa TASAF, na nguvu za Wananchi wa Kijiji cha Kianga Wilaya ya Magharibi A Unguja.
NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Ndg. Abdallah Hassan Mitawi akitowa maelezo ya Kitaalam ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Kianga wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi leo, wakati wa ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, katika Wilaya hiyo, Kituo hicho kimejengwa kupitia Mradi wa TASAF.
 JENGO Jipya la Kituo Cha Afya Kijiji cha Kianga lilijengwa na Tasaf na Nguvu za Wananchi kilichowekwa jiwe la Msingi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, leo akiwa katika ziara yake Wilaya ya Magharibiu A Unguja,leo.(Picha na Ikulu)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...