* Yahimiza uwazi na uwajibikaji kwa taasisi hizo, Serikali yahaidi ushirikiano

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
SERIKALI imehaidi kushirikiana kwa ukaribu zaidi na Serikali ya Uingereza pamoja na asasi za kiraia katika kuhakikisha masuala ya uwazi na uwajibikaji yanaimarika zaidi huku mapambano dhidi ya rushwa yakikomeshwa nchini na hiyo ni baada ya serikali ya Uingereza kupitia shirika lake la maendeleo la kimataifa (The Development for International Development -DFID) kuzindua rasmi mpango mkakati wa miaka 5 wa Uwajibikaji Tanzania ambao umelenga kuzisaidia asasi za kiraia katika kuhamasisha wananchi kushiriki katika masuala ya maendeleo nchini, shughuli iliyofanyika leo katika makazi ya balozi wa Uingereza nchini jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo Msajili na Mkurugenzi wa Idara ya Usajili na Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Neema Mwanga amesema kuwa Serikali inatambua mchango wa azaki katika kujenga jamii mpya licha ya kuwa na changamoto mbalimbali hasa ya baadhi ya maeneo kutofikiwa na huduma zao.

Ameeleza kuwa azaki zitakazopata fungu hilo watumie kwa malengo yaliyopangwa na hiyo ni kwa kuzingatia uwazi na kuwajibika na asasi ambazo hazitafuata matakwa ya sheria zitachukuliwa hatua kali ikiwemo kuzifuta kabisa.

Kwa upande wake Mkuu wa Ofisi ya DFIF nchini Beth Arthy amesema kuwa urafiki baina ya Tanzania na Uingereza umekuwa wa muda mrefu na hiyo inaenda sambamba na kushirikiana katika masuala ya kimaendeleo na mpango huu umelenga kugusa mapambano dhidi ya rushwa, Mabadiliko ya tabia ya nchi, usawa wa kijinsia na ujumuishwaji wa wananchi katika maamuzi ya kimaendeleo na utagharimu takribani shilingi Bilioni 126.

Amesema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakifanya kazi kwa ukaribu zaidi na serikali, taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) pamoja na asasi mbalimbali ambazo zote kwa pamoja zililenga kushirikisha jamii katika shughuli za kimaendeleo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Uhuru Media Ernest Sungura amesema kuwa miradi hiyo ya uwajibikaji inaleta uwazi na uwajibikaji na kupambana na vitendo vya rushwa kama Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Joseph Magufuli inavyotekeleza hayo.

Ameeleza kuwa kupitia vyombo vya habari vya Uhuru vipindi mbalimbali vya uwajibikaji na kupinga rushwa vitaendelea kurushwa na kuchapishwa ili kuzidi kuelimisha Umma zaidi.

Awamu ya kwanza ya mpango huu ulianza rasmi mwaka 2009 hadi 2015 na katika awamu hiyo takribani wananchi milioni 7.5 walifikiwa moja kwa moja na wananchi milioni 22.5 wakifikiwa kwa namna nyingine tofauti.

Na takribani ya jumla ya shilingi Bilioni 392 zilitolewa na kutumika katika ufanyaji maboresho katika kuongeza bajeti ya huduma za kijamii, kuongeza kasi ua ulipaji kodi kwa Serikali, ufuatiliaji, utekelezaji wa Sheria, ugawaji wa ardhi, kupunguza vikwazo masokoni na kuboresha vipato vya Wakulima.

Katika warsha hiyo taasisi mbalimbali za kiraia zilishiriki zikiwemo taasisi ya Wajibu na Haki Elimu.

Msajili na Mkurugenzi wa Idara ya Usajili na Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Neema Mwanga akizungumza kwenye warsha ya uzinduzi wa mpango mkakati wa miaka 5 wa uwajibikaji nchini uliolenga kuwahusisha wananchi kushiriki shuguli za kimaendeleo kupitia asasi za kiraia nchini.
Mkurugenzi mtendaji mkuu wa Uhuru Media Ernest Sungura (katikati) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao wa jamii forum Maxence Melo (kushoto) na Mkurugenzi wa taasisi ya TWAWEZA Aidan Yakuze mara baada ya warsha hiyo leo jijini Dar es salaam.
Msajili na Mkurugenzi wa Idara ya Usajili na Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Neema Mwanga(kulia) akikagua mabanda mbalimbali ya taasisi hizo, pamoja na kupata maelezo ya namna zinazofanya kazi na katika warsha hiyo amewahimiza kufanya kazi kwa kufuata matakwa ya kisheria hasa uwazi na uwajibikaji, katikati ni Mkuu wa Ofisi ha DFIF nchini Berth Arthy.
Msajili na Mkurugenzi wa Idara ya Usajili na Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Neema Mwanga(katikati) akisalimiana na Mkurugenzi mtendaji mkuu wa Uhuru Media Ernest Sungura mara baada ya Warsha hiyo, leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa ofisi ya DFIF nchini Beth Arthy (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi mtendaji mkuu wa Uhuru Media, Ernest Sungura (kulia) mara baada ya warsha hiyo, ambapo Sungura amesema kuwa vipindi vya kupiga vita rushwa vitarushwa na kuchapishwa kupitia vyombo vya habari vya uhuru.
Mkuu wa ofisi ya DFIF nchini Berth Arthy (wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja naMsajili na Mkurugenzi wa Idara ya Usajili na Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Neema Mwanga(wa pili kulia) na Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Uhuru Media Ernest Sungura(kulia) mara baada ya kuzindua rasmi mpango mkakati huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. KIFAFA CHA MIMBA,SABABU ZAKE,DALILI NA MATIBABU
    https://youtu.be/XUw_1ZDg_OU

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...