Na Chalila Kibuda,Globu ya jamii

MJI kasoro bahari!Hivyo ndivyo utasikia baadhi ya wenyeweji wa Mkoa wa Morogoro wakiamua kuuzungumzia mkoa wao ambao umejaaliwa kuwa na kila kitu lakini ukakosa bahari.

Hata hivyo wenyeji hao wanajivunia kuwa na bwawa la maji la Mindu.Ni bwawa marufu sana, ni bwawa ambalo limekuwa na historia ya aina yake na hasa kwa wananchi wanaozunguka bwawa hilo.Ni jambo la kawaida hata kwa wasafiri wanaokuwa kwenye vyombo vya usafiri wakifika katika Bwawa la Mindu kulinyooshea kidole.Utasikia "Umelionaa bwawa la Mindu?Ndio lileeee..."

Uwepo wa bwawa hilo umekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa Manispaa ya Morogoro pamoja na maeneo mengine.Hata hivyo kuna baadhi ya watu hadi leo hii wanaamini bwawa hilo ni la asili kwa maana ya kwamba limekuwepo enzi na enzi.Waamini ni bwawa ambalo hakuna aliyelipeleka zaidi ya Muumba wa mbingu na ardhi.

Ukweli uko hivi pamoja na umaarufu wa bwawa hilo wa muda mrefu pamoja na ukubwa wake wote, ifahamike tu Bwawa hilo la Mindu ambalo katika Manispaa hiyo limechimbwa kuanzia mwaka 1984 hadi 1985 kwa ajili maji katika mji huo kutokana na ukame wa maji katika eneo hilo.

Historia inaeleza kuwa kutokana na ukame uliokuwa katika maeneo hayo ilionekana iko haja ya kuchimbwa bwawa la maji ambalo litakuwa chanzo cha upatikanaji wa maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya kibinadamu.

Hata hivyo kabla ya kuchimbwa kwa bwawa hilo mwaka 1974 ilitungwa sheria ya Usimamizi wa Maji pamoja na mabwawa ili kuweza kusimamia katika sheria.Kutokana na sheria hiyo mwaka 1979 wananchi waliokuwa wakiendesha shughuli za kibidamu katika eneo la Mindu waliwahamisha wananchi kwa ajili ya upishaji Bwawa la Mindu na kuwalipa fidia ili shughuli za kibidamu zisiweze kuingiliana na kusitokee uchafuzi wa maji na udhibiti wa mazingira.

Tangu kuchimbwa kwa bwawa hilo juhudi mbalimbali zimekuwa zikiendelea za kuhakikisha shughuli za kibadamu haziathiri bwawa hilo. Hata hivyo kuongeza kwa idadi ya watu kwenye eneo hilo nako kumefanya baadhi ya watu kutamani kufanya shughuli za kibinadamu pembezoni mwa bwawa hilo.Uzuri ni kwamba wanaosimamia bwawa hilo wako makini na hivyo muda wote wamekuwa wakifuatilia kwa karibu na lengo ni kuona bwawa hilo linabaki kuwa salama kwa maslahi ya wananchi walio wengi.

Hivi karibuni, mawaziri nane wa Serikali ya Awamu ya Tano wakiongozwa na Mwenyekiti wao William Lukuvi ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi walifanya ziara ya kutembelea bwawa la Mindu na kujionea hali halisi ya bwawa hilo ilivyo kwa sasa.

Akizungumza mbele ya mawaziri hao pamoja na maofisa wengine wa ngazi mbalimbali serikalini akiwa eneo la Bwawa la Mindu Ofisa wa Maji wa Bonde la Wami/ Ruvu Mhandisi Simon Ngonyani amesema Bonde la Wami/Ruvu ndio wasimamizi wa vyanzo vya maji kwa kulinda vizazi vya sasa vijavyo hivyo lazima vilindwe kwa gharama yeyote.

Hakusita kueleza kuwa uwepo wa wananchi katika bwawa la Mindu kunahatarisha uwepo wa bwawa hilo ambalo kina chake kimeshapungua na sababu kubwa inatokana na shughuli za kibinadamu zinazoendelea kufanyika.Wananchi wa maeneo hayo wengi wameshindwa kuwa sehemu ya walinzi wa bwawa hilo na baala yake wamekuwa wakiliharibu kwa kufanya shughuli ambazo kimsingi hazikupaswa kufanywa ndani ya eneo hilo la bwawa.

Mhandisi Ngonyani anasema kwa mujibu wa sheria, wananchi wanatakiwa kuwa umbali wa mita 500 kutoka usawa wa bwawa. Aidha amesema katika Bwawa la Mindu kuna watu walifikia hatua kuendesha shughuli za uvuvi na kufanya wananchi hao kuwa na mlipuko wa magonjwa kikiwemo kipindupindu baada ya kuzuia shughuli hizo ugonjwa huo umepungua.

Anafafanua ukweli ni kwamba uwepo wa wananchi katika eneo hilo la bwawa ni hatari kubwa kwani kutokana na mabadiliko ya tabianchi linaweza kupasuka ambapo janga lake litakuwa kubwa kwa wakazi wa Manispaa ya Morogoro na Taifa kwa ujumla.

Mhandisi Ngonyani anasema katika nchi nyingi zenye mabwawa kama hayo wananchi ambao wanaishi karibu nayo wamepata madhara makubwa , hivyo ni vema hatua mbalimbali zikachukuliwa kwa lengo la kuchukua tahadhari ikiwa ni sehemu ya kulinda wananchi.

"Hatuna sababu kuwaacha wananchi wetu katika bwawa la Mindu ni hatari kuwepo kwao,sio kufumbia macho na sheria ipo na fidia walishalipwa kilichofanyika kwa watu waliolipwa waliamua kuwauzia wengine ambapo hawawezi kulipwa fidia,"anasema Mhandisi Ngonyani.

Hata hivyo anasema mbali ya usimamizi wa sheria, anaeleza wazi uwepo wa shughuli za kibidamu ikiwemo kilimo kumeongeza gharama kwa Mamlaka ya Safi na Majitaka Morogoro (Muruwasa) kwa ajili ya kuyatibu maji kwa mahitaji ya asilimia 80 kwa Manispaa Morogoro.

Kutokana na kuwepo kwa changamoto hizo za kisekta na sheria, Rais Dk.John Pombe Magufuli aliunda jopo la mawaziri kwa lengo la kufuatilia changamoto za wananchi ikiwemo kwa waliopo Bwawa la Mindu kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi.

Mwenyekiti wa Jopo la Mawaziri hao, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema kuwa Mamlaka ya Mkoa yahakikishe inasitisha ujenzi wa makazi katika maeneo ya bwawa la Mindu pamoja kuandika barua kwa waziri mwenye dhamana ya maji ili kutoa kibali cha utekelezaji wa sheria kwa wananchi hao.

Pia Lukuvi amesema utekelezaji wa sheria ya kuwaondoa wananchi isitishwe mpaka Waziri atoe kibali.Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Steven Kebwe amesema wananchi wanatengeneza utaratibu wa kutafuta maeneo ya kuwahamishia katika mpango wa upimaji wa viwanja 3000 na kununua kwa fedha ndogo wananchi kuingia au kufanya shughuli yeyote katika chanzo cha maji.

Jopo la Mawaziri hao watapita katika maeneo yenye changamoto katika Mikoa Morogoro, Mbeya, Kigoma, Mara, Geita pamoja na Mwanza na kuja na suluhisho bora ya wananchi katika kuondoa migogoro.Mawaziri hao katika Wizara Ofisi ya Rais-Tamisemi, Kilimo, Ulinzi na Jeshi kujenga Taifa, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano - Mazingira,Maliasili na Utalii,Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Ma kazi,Maji pamoja na Mifugo na Uvuvi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...