Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Mtanange wa Watani wa Jadi Yanga na Simba umemalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa goli 1-0. Mchezo huo ulipigwa leo katika Uwanja wa Taifa kwa kuwakutanisha watani hao wa jadi.

Mechi hiyo ilianza kwa kila upande kumshambulia mpinzani wake kwa zamu bila mafanikio yoyote.Yanga walishindwa kutumia nafasi walizozipata kwenye Kipindi cha kwanza sambamba na watani wao wa jadi.

Mpaka mpira unaenda mapumziko, timu hizo zilienda vyumbani wakitoshana nguvu jwa 0-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa Simba kulisakama lango la Yanga baada ya kufanya mabadiliko kwa kumtoa Kiungo wa Kimataifa kutoka Zambia Clotous Chama na kumuingiza Hassan Dilunga.

Yanga nao walifanya mabadiliko kwa kumtoa mshambuliaji wa Kimataifa raia wa Burundu Amisi Tambwe na nafasi yake kuchukuliwa na Mrisho Ngasa ambapo mabadiliko hayo ya safu ya ushambuliaji wa Yanga ikasalia na Heritier Makambo.

Benchi la ufundi la Yanga likafanya mabadiliko ya kiufundi kwa kumtoa Nahodha Ibrahim Ajib na kumuingiza Mohamed Issa ‘Banka’.Timu hizo ziliendelea kushambuliana kwa zamu ila safu za ulinzi zikiwa makini kila upande na katika Dakika ya 71, mshambuliaji wa Kamataifa wa Rwanda Meddie Kagere akaipatia timu yake goli la kuongoza akitumia madhaifu ya safu ya ulinzi ya Yanga baada ya kukosa maelewano.

Goli hilo liliwapa Simba motisha na kuanza kulisakama lango la Yanga na wapinzani wao Yanga wakijitahidi kutafuta goli la kusawazisha.Mpaka mwamuzi Hance Mabena anamaliza dakika 90 za mchezo huo timu ya Simba inaondoka na ushindi wa goli 1-0 na kujinyakulia alama tatu na kufikisha alama 39 akisalia nafasi ya Tatu ya Ligi.

Na baada ya matokeo hayo Yanga wanakuwa wamepoteza mchezo wa pili wa ligi lakini wakiendelea kusalia katika nafasi ya kwanza kwa alama 58 akifuatiwa na Azam wenye alama 45.

Timu hizo zitacheza mchezo mwingine wa Ligi ambapo Simba watasafiri kwenda Arusha kucheza na African Lyon Feb 19, na Yanga wakielekea Mbao Februari 20.


Kikosi cha Simba kilichoanza.Picha kwa hisani ya Francis Dande).
Kikosi cha Yanga kilichoanza. 
Moja ya hekaheka katika lango la Yanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...