Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakisaini leo jijini Dar es Salaam makubaliano ya mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card) utakaotumika kulipia huduma mbalimbali nchini Tanzania. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakisaini makubaliano ya mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card) utakaotumika kulipia huduma mbalimbali nchini Tanzania. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakibadilishana nakala za makubaliano yao mara baada ya kusaini leo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakibadilishana nakala za makubaliano yao mara baada ya kusaini leo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakionesha nakala za makubaliano ya mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card) utakaotumika kulipia huduma mbalimbali nchini Tanzania. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (kushoto) wakifurahiya jambo mara baada ya kusaini leo jijini Dar es Salaam makubaliano ya mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card) utakaotumika kulipia huduma mbalimbali nchini Tanzania. 
Picha ya pamoja ya viongozi waandamizi wa kampuni zote mara baada ya hafla ya kusaini mkataba huo wa ushirikiano kibiashara. 



SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania TTCL Corporation, kupitia mtandao wake wa huduma za kifedha wa T-PESA pamoja na wadau wa kibiashara, Kampuni tatu kutoka nchini Korea zimesaini mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card).

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika Makao Makuu ya TTCL leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Huduma za T- PESA Ndugu Moses Alponce, alisema mfumo huo unaotumia teknolojia za kisasa ni matokeo ya utafiti uliofanywa na kuonesha mahitaji makubwa ya huduma za malipo yasiyotumia fedha tasilimu. 

Aidha aliongeza kuwa kukamilika kwa mfumo huo kutarahisisha shughuli za kibiashara na kuimarisha uwezo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), katika kukusanya kikamilifu kodi za Serikali kutoka kila miamala itakayofanyika, sambamba na kuongeza ufanisi katika biashara na shughuli nyingine za kiuchumi.

Mfumo huo unaotekelezwa na T-Pesa kwa kushirikiana na wadau wake kibiashara kutoka Jamhuri ya watu wa Korea katika muunganiko wa Kampuni tatu, ambazo ni PayLink Korea, KEH Hana Card pamoja na ATECT & Company unakuwa wa kwanza kuletwa na huduma za fedha kwa kutumia simu za mikononi nchini Tanzania.

"..Kampuni hizi zitashirikiana na T PESA katika zoezi la kuandaa, kupanga na kutengeneza Mfumo wa kadi za NFC na POS Cashless Ecosystem," alisema Alponce.Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee akiwakilisha kampuni hizo alisema kuingia kwa ushirikiano katika mfumo huo utaongeza uwazi katika miamala ya kifedha jambo ambalo litaongeza mapato ya kodi kwenye mifumo ya malipo nchini na kuleta maendeleo.

Ikiwa sasa ni takribani miaka miwili tangu kuanzishwa kwake, T PESA imekuwa na mchango mkubwa katika huduma za Fedha mtandao Nchini, ambapo kwa mujibu wa ripoti ya TCRA toleo la mwaka 2019, T PESA ni moja ya huduma zinazokua kwa kasi kubwa ikiwa na Mawakala 10,000, wateja laki 320,000 wanaozungusha miamala ya takribani Tsh Bilioni 4.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...