Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani akisisitiza jambo katika mkutano huo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Hazina na Uendelezaji Biashara, William Genya akijadiliana jambo na Meneja wa Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) mkoa wa Geita, Glagys Jeffta wanaoshuhudia ni maafisa uendelezaji biashara, Clara Lumbanga, Olivia Musanga Zoka na Phoibe Keu.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Eliud Mwaiteleke akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani leo jioni.
Eneo lililopimwa la Rubambangwe linavyoonekana kwa picha ya Drone,
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Eliud Mwaiteleke, Mkuu wa Wilaya ya Chato Mtemi Simioni na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani wakijadiliana jambo jioni ya leo baada ya uzinduzi wa mauzo ya viwanja Chato.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Eliud Mwaiteleke akijadiliana jambo na Mkuu wa Wilaya ya Geita Josephat Maganga.
 Mazungumzo yakiendelea baada ya uzinduzi wa mauzo ya viwanja.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Eliud Mwaiteleke akijadiliana jambo na  na Kaimu Mkurugenzi wa Masoko wa NHC, Itandula Gambalagi.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani akizungumza kutoa neno la shukurani katika uzinduzi huo kulia kwake ni Mkuu wa Mkuu wa Wilaya ya Chato Injinia Msafiri Mtemi Simioni na kushoto kwake ni Waziri wa Nishati na mbunge wa jimbo hilo, Dk. Medard Kalemani.
Waziri wa Nishati na mbunge wa jimbo hilo, Dk. Medard Kalemani akimshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani kwa mchango wake katika upimaji wa viwanja hivyo vilivyozinduliwa mauzo.


 Hadhira ikifuatilia hafla hiyo ya uzinduzi.
 Hadhira ikifuatilia hafla hiyo ya uzinduzi.
Mkuu wa Wilaya ya Chato Injinia Msafiri Mtemi Simioni  akizunguma katika uzinduzi huo kushoto kwake ni  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani na Waziri wa Nishati na mbunge wa jimbo hilo, Dk. Medard Kalemani. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri na Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya hiyo, Philip Shoni.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani akijadiliana jambo na Waziri wa Nishati na mbunge wa jimbo hilo, Dk. Medard Kalemani.

Waziri wa Nishati na mbunge wa jimbo hilo, Dk. Medard Kalemani akizungumza katika hafla hiyo na kulia kwake ni  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani.


Mkuu wa Wilaya ya Chato Injinia Msafiri Mtemi Simioni akijadiliana jambo na  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani na Waziri wa Nishati na mbunge wa jimbo hilo, Dk. Medard Kalemani.
 Wakifuatilia hafla hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Chato Injinia Msafiri Mtemi Simioni akijadiliana jambo na  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Maulidi Banyani na Waziri wa Nishati na mbunge wa jimbo hilo, Dk. Medard Kalemani.
Wakiagana mara baada ya kuhitimisha hafla ya uzinduzi wa mauzo ya viwanja.


Halmashauri ya Wilaya ya Chato ikishirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) inautangazia umma juu ya uuzaji wa viwanja 1,035 vilivyopimwa na kuwekewa barabara katika eneo la Mlimani na Rubambangwe kata ya Muungano. Mauzo ya viwanja yanaanza wiki ijayo.

Wananchi wote mnakaribishwa kununua viwanja vyenye matumizi mbalimbali kama vile makazi, makazi na biashara, viwanja vya biashara, maeneo ya kumpumzikia, viwanja vya michezo na huduma mbalimbali za kijamii kama zahanati, Shule, Vituo vya Mafuta kwa bei ya kuanzia Tsh 1,300 kwa mita ya mraba.

Viwanja vipo mita chache kutoka katikati ya mji wa Chato. Vipo mkabala na barabara kuu iendayo Bukoba. Pembezoni mwa Ziwa Victoria.

Viwanja vilivyopimwa na kupangwa kwa ajili ya makazi vina ukubwa kama ifuatavyo:
1. Ujazo wa juu (High density)
2. Ujazo wa kati (Medium density)
 3. Ujazo wa chini (Low density) 

VIWANGO VYA GHARAMA YA VIWANJA KWA MATUMIZI MBALIMBALI

1. Makazi –Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 1,300/=
2. Makazi na biashara- Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 1,700/=
3. Biashara (Hotel, Vituo vya mafuta, maduka makubwa)- Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 2,200/=
4. Huduma za jamii (Zahanati, shule ya awali, sekondari) Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 2,200/=
5. Ibada/kuabudu- Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 2,200/=

UTARATIBU WA KUNUNUA KIWANJA

Chukua fomu ya maombi kutoka o­fisi za Halmashauri ya Wilaya ya Chato au Ofi­si ya NHC iliyo karibu nawe.
Lipia angalau asilimia 30 ya thamani ya kiwanja unachonunua na kiasi kinachobaki kilipwe ndani ya siku 90.
Malipo yote yafanyike kwenye akaunti ya benki ifuatayo: Jina la Akaunti : MRADI WA VIWANJA CHATO Nambari ya akaunti : 327 100 116 07 Benki: NMB Tawi la Chato
Rejesha fomu ya maombi uliyojaza kwa usahihi ukiambatanisha pamoja na vielelezo vinavyohitajika ikiwemo nakala ya malipo (deposit slip) kutoka benki.
Utapatiwa barua ya uthibitisho (Offer Letter) mara tu ombi lako litakapokubaliwa, pamoja na masharti ya kukamilisha malipo ya kiwanja unachochagua.
Kwa maelezo zaidi tembelea ofisi za Idara ya ardhi ya Halmashauri ya Wilaya ya Chato.

Au KAMBARAGE House, 1 Mtaa wa Ufukoni, Dar es Salaam, Tanzania. Kwa Mawasiliano piga namba  +255 282 228 007/ +255 754 444 333.

PHILIP SHONI
KWA NIABA YA MKURUGENZI MTENDAJI
HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
21/02/2019

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...