Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Eliud Mwaiteleke akijadiliana jambo na na Kaimu Mkurugenzi wa Masoko wa NHC, Itandula Gambalagi.
Wakifuatilia hafla hiyo.
Wakiagana mara baada ya kuhitimisha hafla ya uzinduzi wa mauzo ya viwanja.
Halmashauri
ya Wilaya ya Chato ikishirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)
inautangazia umma juu ya uuzaji wa viwanja 1,035 vilivyopimwa na kuwekewa
barabara katika eneo la Mlimani na Rubambangwe kata ya Muungano. Mauzo ya
viwanja yanaanza wiki ijayo.
Wananchi
wote mnakaribishwa kununua viwanja vyenye matumizi mbalimbali kama vile makazi,
makazi na biashara, viwanja vya biashara, maeneo ya kumpumzikia, viwanja vya
michezo na huduma mbalimbali za kijamii kama zahanati, Shule, Vituo vya Mafuta
kwa bei ya kuanzia Tsh 1,300 kwa mita ya mraba.
Viwanja
vipo mita chache kutoka katikati ya mji wa Chato. Vipo mkabala na barabara kuu
iendayo Bukoba. Pembezoni mwa Ziwa Victoria.
Viwanja
vilivyopimwa na kupangwa kwa ajili ya makazi vina ukubwa kama ifuatavyo:
1.
Ujazo wa juu (High density)
2.
Ujazo wa kati (Medium density)
3. Ujazo wa chini (Low density)
VIWANGO
VYA GHARAMA YA VIWANJA KWA MATUMIZI MBALIMBALI
1.
Makazi –Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 1,300/=
2.
Makazi na biashara- Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 1,700/=
3.
Biashara (Hotel, Vituo vya mafuta, maduka makubwa)- Bei ya kiwanja kwa mita moja
ya mraba ni Shilingi 2,200/=
4.
Huduma za jamii (Zahanati, shule ya awali, sekondari) Bei ya kiwanja kwa mita
moja ya mraba ni Shilingi 2,200/=
5.
Ibada/kuabudu- Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 2,200/=
UTARATIBU WA KUNUNUA KIWANJA
Chukua
fomu ya maombi kutoka ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Chato au Ofisi ya NHC
iliyo karibu nawe.
Lipia
angalau asilimia 30 ya thamani ya kiwanja unachonunua na kiasi kinachobaki
kilipwe ndani ya siku 90.
Malipo
yote yafanyike kwenye akaunti ya benki ifuatayo: Jina la Akaunti : MRADI WA
VIWANJA CHATO Nambari ya akaunti : 327 100 116 07 Benki: NMB Tawi la Chato
Rejesha
fomu ya maombi uliyojaza kwa usahihi ukiambatanisha pamoja na vielelezo
vinavyohitajika ikiwemo nakala ya malipo (deposit slip) kutoka benki.
Utapatiwa
barua ya uthibitisho (Offer Letter) mara tu ombi lako litakapokubaliwa, pamoja
na masharti ya kukamilisha malipo ya kiwanja unachochagua.
Kwa
maelezo zaidi tembelea ofisi za Idara ya ardhi ya Halmashauri ya Wilaya ya
Chato.
Au
KAMBARAGE House, 1 Mtaa wa Ufukoni, Dar es Salaam, Tanzania. Kwa Mawasiliano
piga namba +255 282 228 007/ +255 754
444 333.
PHILIP SHONI
KWA NIABA YA MKURUGENZI MTENDAJI
HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
21/02/2019
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...