Mnamo tarehe 11.02.2019 majira ya saa 23:45 usiku huko eneo la Soweto, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilikamata gari lenye namba za usajili T.937 CKD aina Toyota Saloon likiwa na vipodozi vya aina mbalimbali vilivyopigwa marufuku nchini. Vipodozi vilivyokamatwa ni:- 
Extra Clair katoni nane [08].
Perfect White katoni mbili [02].
Epiderm Cream dazani arobaini na saba [47]
Diproson dazani ishirini na moja [21]
Coco Pulp katoni mbili [02]
Carolight katoni sita [06]
Citro Light katoni tatu [03]
Teint Clair katoni mbili [02]
Top Lemon katoni nne [04]
Clair Men katoni mbili [02]
Princes Clair katoni nne [04]
Movet boksi mbili [02]
Miki Clair katoni mbili [02]
Top Clair Plus katoni moja [01]
Collagen formula boksi mbili [02]
Mont Clair boksi mbili [02]
Movet tube pcs mbili [02]
Movet boksi mbili [02]
Cocoderm boksi moja [01] 

KUPATIKANA NA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU NCHINI. 

Mnamo tarehe 12.02.2019 majira ya saa 07:15 asubuhi huko eneo la Check Point Igurusi, Kata ya Igurusi, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali na Mkoa wa Mbeya, Polisi wakiwa doria walimkamata SAID IDDY @ MOHAMED [32] Dereva na Mkazi wa Mbadula Arusha akiendesha gari lenye namba za usajili T.298 DCH aina ya Scania Basi la abiria – HAJI’s akitokea Mbeya kuelekea Arusha akiwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku nchini aina mbalimbali. 

Vipodozi vilivyokamatwa ni:- 
Diana Boksi mbili [02].
White Max Boksi tatu [03].
Secret White Location Boksi moja [01] 

Upelelezi unaendelea na mara baada ya kukamilika, mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani. 


KUPATIKANA NA SILAHA [GOBORE] BILA KIBALI. 

Mnamo tarehe 11.02.2019 majira ya saa 14:35 mchana huko eneo la Makasini – Uyole, Kata ya Uyole, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi walimkamata PAUL ABRICK [66] Mkazi wa Mtaa wa Nyahoro – Uyole akiwa na silaha Gobore aina ya Tower yenye namba 1878 bila kibali. Upelelezi unaendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...