Na Andrew Chale

Viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo Mawaziri pamoja na viongozi wengine wamejitokeza kuhani msiba wa mtoto wa Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia Mbunge wa Nzega Vijijini  Dk.Hamisi Andrea  Kigwangalla  marehemu Zulqarinain  aliyefariki jana February 21,2019 majira ya Saa nne asubuhi  JAKAYA KIKWETE CARDIAC INSTITUTE - MUHIMBILI.

Viongozi hao pamoja na ndugu na jamaa na marafiki wamejumuika kwa pamoja nyumbani kwake Mikocheni A katika Kota za Mawaziri jirani na kituo cha mafuta cha Victoria.

Baadhi ya viongozi hao akiwemo Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Paramagamba Kabudi,Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii  Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu,Waziri wa Kilimo  Japhet Hasunga

Wengine ni Naibu Waziri wa Afya  Dk Faustine Ndugulile, Naibu waziri mambo ya ndani Masauni, Naibu Waziri Madini, Naibu Waziri mambo ya Nje  na wengine wengineo.

Pia wengine Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda pamoja na wengine wakiwemo Wabunge,  ndugu  jamaa na Marafiki.

Awali  Msemaji wa Familia Bwana  Lumola alieleza  kuwa mwili utasafirishwa 22 Februari kwa  ndege na Mazishi yanatarajiwa kufanyika saa Kumi jioni Nzega Vijijini  Jimboni kwa Waziri Dk Kigwangalla.

#R.I.P. Zul.

Inna lillahi wainna illaihi rajiuun







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...