Katibu wa Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Jason Rweikiza(kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu miswada ambayo imejadiliwa bungeni.
Mbunge wa Mbinga Mjini Sixtus Mapunda akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu umuhimu wa Sheria ya Vyama vya Siasa

*Wazungumzia umuhimu wa Sheria ya Vyama vya Siasa na faida zake kwa Watanzania 

 Na Said Mwishehe,Globu ya jamii 

 WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) wameazimia kufafanua mambo mbalimbali ambayo yalijiri katika vikao vya Bunge ambalo limemalizika vikao vyake Bungeni Mjini Dodoma hivi karibuni. Kwa mujibu wa Katibu wa Wabunge hao Jason Rweikiza pamoja na mambo mengine wamejikita kuzungumzia miswaada sita ambayo imepitishwa na Bunge hilo na kufafanua kuhusu Sheria ya vya siasa kwa undani zaidi ili umma wa Watanzania ufahamu kinagaubaga. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Rweikiza amesema wameona ni vema wakafafanua mambo mbalimbali yakiwemo ya Sheria ya Vyama vya siasa iliyopitishwa kwenye vikao hivyo kwasababu inaonesha wananchi wengi sio tu hawajahifahamu sawasawa bali pia kuna upotoshaji mwingi.

 "Wabunge wa CCM kwa umoja wetu tumedhamiria kuufahamisha umma kuhusu mambo ambayo yamejadiliwa bungeni , na hasa miswada sita ambayo imepitishwa na kuwa sheria.Tanalojukumu la kuhahakikisha Watanzania wanafahamu vema kila ambacho kimejadiliwa bungeni kwani wabunge tunaotokana na Chama hiki tunayo dhamana ya kuelezea kwa ufasaha mambo yanavyokwenda,"amesema Rweikiza. 

Amefafanua Bunge lilimalizika mwishoni mwa wiki iliyopita lilikuwa mahususi kwa ajili ya kupokea taarifa mbalimbali kutoka Kamati za Bunge ikiwemo miswada sita ambayo imepitishwa."Tumekuja kwenu waandishi wa habari tukiamini mtakuwa daraja la kufikisha haya tunayoyazungumza kwa wananchi." 

Akizungumzia zaidi kuhusu Sheria ya Vyama vya Siasa, Mbunge wa Mbinga Mjini Sixtus Mapunda amesema sheria hiyo ni muhimu kwani sasa Chama cha siasa ambacho kitaanzishwa kitakuwa kinazingatia maslahi mapana ya nchi yetu badala ya kuwa chama cha mfukoni au cha kifamilia. "Ni ukweli usiopinginga kuna vyama hapa vya siasa ambavyo namna vinavyoendeshwa si kwa ajili ya maslahi mapana ya Watanzania bali ni vyama kwa ajili ya kunufaisha watu na familia zao.

Hivyo ujio wa Sheria ya Vyama vya Siasa utasaidida kuweka mambo sawa na kuwa na Chama cha siasa ambacho kitakuwa kimezingatia mambo yote muhimu ambayo yanatambulika kwa mujibu wa sheria hiyo,"amesema. 

Amefafanua kuwa wameona umuhimu wa kuzungumzia sheria hiyo pamoja na nyingine kwa kuwa wao ndio wenye Serikali na ndio watakaobeba lawama siku mambo yakiharibika."Tumekutana nanyi hapa leo hii kufafanua mambo yalijiri bungeni maana hatutaki kuona wengine wakipotosha, hivyo ni jukumu letu kuwaambia ukweli ili umma ujue." 

Mapunda amesema tangu nchi yetu iingie kwenye mfumo wa Vyama vingi tumefikisha miaka 26 na katika kipindi chote hicho kuna mambo mengi kama Taifa limejifunza na hivyo sasa wameamua kuja na Sheria ambayo itaimatisha vyama vya siasa na hasa kuwa kama taasisi inayoeleweka na sio kuwa na vyama vya siasa ambavyo ni vya mifukoni.

 "Tumeshuhudia malalamiko mengi kutoka kwenye baadhi ya vyama vya siasa , kumekuwepo na malalamiko ya matumizi ya fedha.Kuna vyama vya siasa imefikia mahali Mwenyekiti anakopesha fedha kwa chama.Kupitia Sheria ya Vyama vya Siasa inakwenda kuweka utaratibu mzuri wa namna gani chama cha siasa kinatakiwa kuendeshwa,"amesema Mapunda na kuongeza Watanzania wasikubali kupotoshwa kuhusu sheria hiyo. 

 Wakati huo huo Mbunge wa Mlalo mkoani Tanga Rashid Shangazi ametumia nafasi hiyo kuzungumzia hatua ya baadhi ya mapori kupandishwa hadhi na kuwa hifadhi za Taifa ambapo mbali ya kutunza na kuhifadhi mazingira, ni fursa muhimu kwa wawekezaji kuwekeza katika hifadhi hizo kwa kujenga hoteli za kitalii. 

Ametaja hifadhi hizo ni hifadhi ya Taifa Burigi, Kimisi, Biharamulo, Ibanda na Chief Rumanyika ambapo amesema pia ni vema TANAPA wakakaa na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kuangalia namna ya kuangalia namna gani wanaweza kuweka mazingira mazuri ya msamaha wa kodi kwa baadhi ya vifa kwani TANAPA watakuwa na jukumu la kujenga miundombinu mbalimbali kwenye hifadhi hiyo. 

 Pamoja na mambo mengine wabunge hao wa CCM wametoa ufafanuzi kuhusu madai ya kupotea kwa fedha Sh.trilioni 1.5 ambapo wamefafanua madai hayo hakuna ukweli wowote bali kuna moja wa Bunge anachokifanya ni kupotosha umma. Wabunge hao wamesema hata Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) imethibitisha hakuna upotevu wa fedha hizo na hivyo wamewahakikishia Watanzania kupuuza madai ya uwepo wa upotevu wa fedha hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...