Wananchi wameshauriwa kutokukaa kimya  pindi wanapopokea ujumbe wa matapeli bali waripoti Polisi  namba iliyokutuma ujumbe huo ili jeshi hilo  ilifanyie kazi.

Ushauri huo umetolewa na mkuu wa kitengo cha makosa ya kimtandao mkoa wa Arusha Inspekta Aman Ngaleni alipokuwa akitoa elimu kwa wananchi waliohudhuria  Kampeni ya Mnada Kwa Mnada, karibu Tukuhudumie inayoendeshwa kwa ushirikiano kati ya Mamlaka ya Mawasiliano TCRA, Jeshi la Polisi kitengo cha uhalifu mitandaoni, makampuni ya siku ya Vodacom, Tigo, Airtel, Halotel, Zantel na TTCL.

Kampeni hiyo imefanyika Februari 20, 2019 katika viwanja vya stendi ya Kilombero, jijini Arusha.
 Wananchi  wakipata huduma katika kampeni ya Mnada kwa Mnada katika Stendi ya Kilombelo Jijini Arusha ikiwa kampeni ya TCRA kuelimisha wananchi kuhusiana na huduma za mawasiliano zinazotolewa na wadau mbalimbali.
 Wadau wakijadiliana masuala ya Mawasiliano katika kampeni ya Mnada kwa Mnada katika stendi ya Kilombelo Jijini Arusha.
Mwananchi akisoma jarida la Kituo cha Daladala cha Kilombelo Jijini Arusha katika  Kampeni  ya Mnada kwa Mnada  inayoendeshwa na Mamlaka ya Makatika St kuelimisha mawasiliano (TCRA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...