Wananchi wameshauriwa kutokukaa kimya pindi wanapopokea ujumbe wa matapeli bali waripoti Polisi namba iliyokutuma ujumbe huo ili jeshi hilo ilifanyie kazi.
Ushauri huo umetolewa na mkuu wa kitengo cha makosa ya kimtandao mkoa wa Arusha Inspekta Aman Ngaleni alipokuwa akitoa elimu kwa wananchi waliohudhuria Kampeni ya Mnada Kwa Mnada, karibu Tukuhudumie inayoendeshwa kwa ushirikiano kati ya Mamlaka ya Mawasiliano TCRA, Jeshi la Polisi kitengo cha uhalifu mitandaoni, makampuni ya siku ya Vodacom, Tigo, Airtel, Halotel, Zantel na TTCL.
Kampeni hiyo imefanyika Februari 20, 2019 katika viwanja vya stendi ya Kilombero, jijini Arusha.
Wananchi wakipata huduma katika kampeni ya Mnada kwa Mnada katika Stendi ya Kilombelo Jijini Arusha ikiwa kampeni ya TCRA kuelimisha wananchi kuhusiana na huduma za mawasiliano zinazotolewa na wadau mbalimbali.Wadau wakijadiliana masuala ya Mawasiliano katika kampeni ya Mnada kwa Mnada katika stendi ya Kilombelo Jijini Arusha.
Mwananchi akisoma jarida la Kituo cha Daladala cha Kilombelo Jijini Arusha katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada inayoendeshwa na Mamlaka ya Makatika St kuelimisha mawasiliano (TCRA).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...