Waziri wa Madini, Doto Biteko (pichani) amefungua warsha ya siku mbili kuanzia leo Februari 11, 2019 kwa wadau wa madini inayolenga kujadili maudhui ya kanuni mpya za uanzishwaji masoko ya madini kama alivyoagiza Rais Dkt. John Pombe Magufuli hivi karibuni.

Warsha hiyo inayofanyika Jijini Mwanza imeandaliwa na Wizara ya Madini kupitia uratibu wa taasisi ya Uongozi Institute na kuwashirikisha wadau na viongozi mbalimbali kutoka mikoa 12 nchini. 
Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa watu kushoto waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimali akiwemo Katibu Mkuu Tume ya Madini, Profesa Simon Msanjila, (wa pili kushoto waliokaa), Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mulabwa (wa kwanza kushoto waliokaa) na Wakuu wa Wilaya zilizoshiriki warsha hiyo. 

Wengine waliokaa ni Mkuu wa Wilaya Misungwi, Juma Sweda (wa pili kulia) aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza pamoja na Mkuu wa Idara ya Mafunzo kwa Viongozi kutoka taasisi ya UONGOZI Institute, Kadari Singo (wa kwanza kulia) aliyemwakilisha Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashari za Wilaya zilizoshiriki warsha hiyo.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na Makatibu Tawala kutoka wilaya zilizoshiriki warsha hiyo.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa wizara hiyo.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa wachimbaji wadogo wa madini.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa taasisi ya UONGOZI Institute.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...