WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa akizungumza baada ya kupokea taarifa ya mkoa wa Tanga wakati wa ziara yake leo
WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kushoto akimsikiliza kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi wakati akielezea hali ya upatikanaji wa maji kwa mkoa wa Tanga wakati wa ziara yake
WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kulia akisaini kitabu cha wageni wakati alipofika Ofisi za Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Mhandisi Geofrey Hilly



WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa ameagiza taasisi zote za serikali zifungiwe mita za luku ili ziweze kwenda na matumizi mazuri ya maji ili kupunguza changamoto za kutokulipa kwa wakati bili za maji na kujikuta zikiingia kwenye madeni makubwa.

Proffesa Mbarawa aliyasema hayo leo wakati wa ziara yake mkoani Tanga ambapo alisema mita za luku litasaidia kuweza kuondokana na kasumba za watu kumwaga maji hivyo na hivyo kuweza kusimamia matumizi ya maji kwenye maeneo yao.

“Ndugu zangu mita za luku msiwapelee wateja sugu bali wapelekeeni hata wale watu wengine ambao wapo kwenye maeneo mbalimbali lakini pia Jeshi la Polisi sio wabaya wanalipa bili lakini wawekeeni mita za luko isipokuwa ndani ya kituo cha Polisi msiweke”Alisema Waziri Mbarawa.

“Lakini hatupelekei wateja sugu tunakosea kwa sababu hii inaweza kupelekwa kukote kwa sababu inaweza kusimamia matumizi ya maji ndani ya mwezi husika…..nirudir Jeshi la Polisi sio wabaya wanalipa bili zao lakini wawekeni mita sio mwanzo maeneo mengi Mtwara,,Iringa nao wanatumiakwenye kota zao wawekeeni mita hizo”Alisema Waziri Mbarawa.Aidha pia mita hizo la luku zitaweza kusaidia kuweka matumizi mazuri ya maji na mambo ya kuanza kulalamika hawalipi tuwafungie traasisi zio nyingi mita moja laki mbili ukchukua wateja 20 karibuni milioni nne na mapato yatakayopatikana ni makubwa.

Hata hivyo alsema serikali imejipanga kuhakikisha changamoto ya huduma ya maji hapa nchini inatatuliwa ili wananweza waweze kunufaika na huduma hiyo muhimu kwa ukuaji wa uchumi na maendeleo.Katika ziara hiyo Waziri Mbarawa alitembelea maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye chanzo cha Maji cha Mabayani,Mtambo wa kusafirishia maji eneo la Mowe na eneo la Horohoro wilayani Mkinga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...