Na Editha Karlo wa blog ya jamii,Kigoma.
WAZIRI Mkuu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania mhe Kassim Majaliwa amewasili leo Mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi ya siku nne.
Lengo la ziara yake imeelezwa kuwa ni kuweka msisitizo katika ufufuaji na uendelezaji wa zao la chikichi ikiwa ni pamoja na kukagua vitalu vya mashamba ili kuliboresha zaidi zao hilo.
Aidha katiaka ziara yake,Waziri Mkuu atatembelea katika Wilaya ya Kigoma Uvinza,Kibondo na Kakonko,sambamba na kuitembelea kambi ya wakimbizi ya Nduta iliyopo Wilayani kibondo na kuzungumza nao.
Waziri
Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana na mkuu wa Mkoa
wa Kigoma Brigedia Jenerali Emanuel Maganga baada ya kuwasili katika
uwanja wa ndege kigoma
Waziri
Mkuu Kassimu Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali
Hosea Ndagala baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kigoma
Waziri mkuu akifurahi pamoja na kikundi cha ngoma cha akina mama
Waziri
mkuu Kassimu Majaliwa akiwasalimia wananchi waliofika kumlaki katika
uwanja wa ndege wa kigoma, baada ya kuwasili kwaajili ya ziara ya
kikazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...