Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
SERIKALI nchini kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewahakikishia wafugaji kuwa hakuna mifugo itakayopotea kutokana na magonjwa mbalimbali.
Haya yameelezwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdullah Ulega wakati akizungumza na wafugaji wa Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani, wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja alioifanya mkoani humo kwa lengo la kukagua miradi iliyoko chini ya wizara hiyo.
Amesema Serikali ilibinafsisha sekta hiyo kwa watu binafsi,lakini kwa sasa imerejeshwa serikalini ili kuwasaidia wafugaji wa aina zote.
"Kwa sasa tunazalisha chanjo ya mdondo zaidi ya milioni 100 kwa mwaka,lengo ni kuwafanya wafugaji wa kuku na hasa akinamama waweze kuondokana na umasikini,"amesema Ulega.
Ameongeza madhumuni ya Serikali ya Awamu ya tano ni kuhakikisha nchi inakuwa na mifugo mizuri yenye kuleta tija kwa wafugaji na wawekezaji wa nyama,hivyo amewataka wafugaji kuamini serikali kwa jinsi inavyowapambania katika kuhakikisha soko la bidhaa hiyo inakuwa kubwa na yenye tija kwao.
Aidha ameongeza kuwa kipindi hiki wafugaji nchini wamekuwa wakinyanyaswa na wafanya biashara kwa kuuza chanjo hizo kwa bei ya Sh.35,000 mpaka Sh. 45,000 kutokana na hali hiyo Serikali imeamua kusambaza dawa hizo za chanjo kwa bei ya Sh.20,000, hivyo itawasaidia watanzania wengi na kuondoa vifo vya mifugo.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa wlWakala maabara ya vetenari Tanzania,Dk. Furaha Mramba amesema chanjo zinazozalishwa katika maabara hiyo zinaubora uliothibitishwa na mamlaka za maabara za Mifugo Africa na itakapokamilika itatosheleza mahitaji ya ndani na nyingine kuuzwa nje ya nchini.
Katika ziara hiyo Ulega pia ametembelea chamba la kuzalisha malisho ya mifugo lililopo Vikuge wilayani Kibaha, pamoja Halmashuri ya Chalinze wilayani Bagamoyo kisha kuhutubia mkutano wa hadhara kata ya Pangani na kuwaomba wakazi wa kata hiyo kuacha tabia ya kuvamia maeneo yaliotengwa na serikali kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Maendeleo.
SERIKALI nchini kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewahakikishia wafugaji kuwa hakuna mifugo itakayopotea kutokana na magonjwa mbalimbali.
Haya yameelezwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdullah Ulega wakati akizungumza na wafugaji wa Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani, wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja alioifanya mkoani humo kwa lengo la kukagua miradi iliyoko chini ya wizara hiyo.
Amesema Serikali ilibinafsisha sekta hiyo kwa watu binafsi,lakini kwa sasa imerejeshwa serikalini ili kuwasaidia wafugaji wa aina zote.
"Kwa sasa tunazalisha chanjo ya mdondo zaidi ya milioni 100 kwa mwaka,lengo ni kuwafanya wafugaji wa kuku na hasa akinamama waweze kuondokana na umasikini,"amesema Ulega.
Ameongeza madhumuni ya Serikali ya Awamu ya tano ni kuhakikisha nchi inakuwa na mifugo mizuri yenye kuleta tija kwa wafugaji na wawekezaji wa nyama,hivyo amewataka wafugaji kuamini serikali kwa jinsi inavyowapambania katika kuhakikisha soko la bidhaa hiyo inakuwa kubwa na yenye tija kwao.
Aidha ameongeza kuwa kipindi hiki wafugaji nchini wamekuwa wakinyanyaswa na wafanya biashara kwa kuuza chanjo hizo kwa bei ya Sh.35,000 mpaka Sh. 45,000 kutokana na hali hiyo Serikali imeamua kusambaza dawa hizo za chanjo kwa bei ya Sh.20,000, hivyo itawasaidia watanzania wengi na kuondoa vifo vya mifugo.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa wlWakala maabara ya vetenari Tanzania,Dk. Furaha Mramba amesema chanjo zinazozalishwa katika maabara hiyo zinaubora uliothibitishwa na mamlaka za maabara za Mifugo Africa na itakapokamilika itatosheleza mahitaji ya ndani na nyingine kuuzwa nje ya nchini.
Katika ziara hiyo Ulega pia ametembelea chamba la kuzalisha malisho ya mifugo lililopo Vikuge wilayani Kibaha, pamoja Halmashuri ya Chalinze wilayani Bagamoyo kisha kuhutubia mkutano wa hadhara kata ya Pangani na kuwaomba wakazi wa kata hiyo kuacha tabia ya kuvamia maeneo yaliotengwa na serikali kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Maendeleo.
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na watumishi
mbalimbali wa kampuni ya Ranchi ya Taifa ya Mlandizi wilaya ya Kibaha
Mkoa wa Pwani.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akifafanua jambo kwenye
mkutano wa hadhara kata ya Pangani,ambapo amewaomba wakazi wa kata hiyo
kuacha tabia ya kuvamia maeneo yaliotengwa na
serikali kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Maendeleo.(Picha na Emmanuel
Massaka,MMG)
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega (alienyosha mkono)
akiwa ameambatana na watendaji mbalimbali wakikagua upanuzi
mkubwa wa maabara ya kutengenezea chanjo
za kudhibiti magonjwa ya mifugo iliyopo mji wa Kibaha mkoa wa Pwani.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na wafugaji ambapo aliwahakikishia kuwa hakuna
Mifugo itakayopotea kutokana na ugonjwa wowote.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega(katikati) akiwa katika picha ya pamoja.
Muonekano wa Kiwanda cha chanjo ya Hester Biosciences kinachojengwa kata ya Tangini wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani.(Picha zote na Emmanuel Massaka,MMG)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...