Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro amekabidhi mabwawa manne makubwa yenye uwezo wa kuhifadhi na kuvuna maji ya Mvua Milioni Thelathini na nane za maji ya mvua kwa Viongozi wa kata ya OLDONYOSAMBU ambao wengi wao wanatoka katika maeneo ya Wafugaji kwa ajili ya matumizi yao na mifugo katika kijiji cha LEMANDA.
Dc Muro amekabidhi Mabwaya hayo , mara baada ya kuyapokea kutoka kwa wadau wa maendeleo Shirika la OIKOS la nchini Italia kwa ufadhili wa Umoja wa Mataifa ( EU ) Pamoja na ushirikiano wa nguvu za ofisi ya mkuu wa wilaya ya Arumeru pamoja na wananchi wa Halmashauri ya Arusha Dc.
Awali Mabwawa hayo yalikuwa na uwezo wa kukusanya ma kuhifadhi maji lita milioni sita tu na sasa yamekarabatiwa na kutengenezwa kuweza kumudu kuhifadhi maji lita million 38, pamoja na ujenzi wa Mapalio ya kisasa ya kunyweshea maji mifugo inayotoka katika maeneo mbalimbali mkoani Arusha
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro akiongea na Wafugaji katika kijiji cha Lemada.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro akijumuika kucheza ngoma na Wafugaji katika kijiji cha Lemada.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro akijumuika kucheza ngoma na Wafugaji katika kijiji cha Lemada.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro akifurahia zawadi alizopata katika kijiji cha Lemada.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro akikagua moja ya mabwawa manne katika kijiji cha Lemada.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro akikagua moja ya mabwawa manne katika kijiji cha Lemada.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro na ujumbe wake wakitembelea miradi ya wafugaji katika kijiji cha Lemada.
Moja ya mabwawa manne katika kijiji cha Lemada.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...