Na Ahmed Mahmoud,Arusha.
Diwani wa Kata ya Lemara ,Profesa Raymond Mosha ameanzisha mpango wa kuwafikia watu wenye ulemavu na kuwapatia mahitaji yao pamoja na nyenzo wanazohitaji ikiwemo baiskeli maalumu za walemavu.
Akizungumza katika zoezi la kukabidhi baiskeli ya mlemavu mwenye umri wa miaka zaidia ya sitini mkazi anayeitwa Mzee George Makinda  wa kata ya Lemara katika eneo la Njiro jijini Arusha amesema kuwa  baiskeli  hiyo  itamsaidia kujishughulisha na kazi zake kama kawaida.
Msaada wa baiskeli hiyo  imetolewa na Professa Raymond Mosha ambae ni diwani wa kata hiyo ya Lemara baada ya kuona familia ya Mzee George Makinda haina uwezo wa ununuzi wa baiskeli hiyo,
Professa Mosha alisema kuwa alihuzunishwa sana na maisha ya mlemavu huyo kwani George Makinda  miaka ya nyuma alikua mzima lakini alikubwa na ugonjwa wa kupooza uliomfanya kua mlemavu wa kushindwa kuongea wala kutembea.
alisema hali hiyo ndio iliomgusa yeye na marafiki zake nakuamua kujitolea baiskel ambayo itamsaidia kwa namna moja au nyingine kutembelea na kujiona kama watu wengine.
Hata hivyo Mke wa Mzee George Makinda  Bi Estar Makinda  pamoja na kutoa shukurani  ya  msaada wa Baiskel hiyo ambayo anataja kua sababu ya kumfanya kumpa ahuweni kwakua ameteseka kwa muda mrefu katika kumlea mumewe,
Estar alisema hata muda mwingine alishindwa kujishughulisha na kazi za kiuchumi nakubaki kumhudumia mumewe  kutokana na  muda wote ni mtu wa kuhudumiwa kila kitu,
“ sasa amepatiwa msaada wa Baisekel itakayomsaidia kutembea naamini sasa mabadiliko ya familia yataonekana”  Alisema Estar Makinda.
Diwani wa kata ya Lemara Profesa  Raymond Mosha akikabidhi baiskeli ya walemavu kwa mkazi wa kata hiyo George Makinda ambaye ni mlemavu wa miguu baada ya kupata ugonjwa wa kupooza .picha zota na Mahmoud Ahmad Arusha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...