* Waziri Mkuu kutangaza sheria mpya ya umiliki wa silaha ndani ya siku 10
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
LEO Machi 20 ndugu wa familia za waliopoteza maisha katika shambulio la kigaidi katika misikiti ya Wood na Al Nool katika mji wa Christchurch nchini Newzealand.

Kwa mujibu wa mtandao wa Dailymail miili hiyo imekabidhiwa kwa ndugu zao huku polisi wakieleza kuwa uchunguzi umekamilika ambapo miili 12 ikiwa imetambulika na tayari miili 6 imekabidhiwa kwa ndugu zao.

Waziri Mkuu nchini humo Jacinda Ardern amesema kuwa kufikia jumatano miili yote itakuwa imekabidhiwa kwa ndugu zao.

Aida Jacinda amesema kuwa ndani ya siku 10 kuanzia sasa sheria mpya ya umiliki wa silaha itatangazwa na wanaamini taifa hilo litakuwa salama zaidi.

Shambulio hilo la kigaidi lilitokea ijumaa wiki iliyopita na tayari mtuhuma wa mauaji hayo Brenton  Tarrant (28)raia wa Australia alifikishwa mahakama mapema Jumamosi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...