Na Mwandishi wetu Mihambwe
Afisa Tarafa Mihambwe Gavana Emmanuel Shilatu ameshiriki ujenzi wa Zahanati ya Ngongo iliyopo Kijiji Cha Ngongo kilichopo kata ya Michenjele.
Gavana Shilatu alienda kufuatilia utekelezaji wa maagizo yake ya ujenzi wa mradi huo wa Zahanati alioagiza ndani ya siku mbili uanze kutokana na kutelekezwa tangu Mwaka jana.
Gavana Shilatu alifurahishwa kukuta nyasi zimefyekwa na Mafundi wapo kazini Kama alivyoagiza na kuwasisitiza watangulize mbele uzalendo kwa kuhakikisha mradi unajengwa kwa kuzingatia ubora na viwango vinavyolingana na thamani ya pesa.
Katika ushiriki wa ujenzi huo Gavana Shilatu aliambatana na Serikali ya Kijiji pamoja na kamati ya ujenzi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...