Wakati ujenzi wa barabara ya Mpemba hadi Isongole Ileje mkoani Songwe ukiendelea shule za Msingi na Sekondari tayari zimeonja matunda ya mradi huo
kwa kumwagiwa vifaa vya michezo,madawati pamoja na redio za kisasa kwajili ya
matumizi ya wanafunzi.
Kampuni ya Kichina GEO Company iligawa vifaa hivyo ikiwa ni
kujibu kwa vitendo ombi la Mkuu wa Wilaya hiyo Ndugu Joseph Mkude baada ya
kuendelea kupokea kero ya kukosekana kwa vifaa hususani vya michezo kwa shule
zake.
Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali
Nicodemas Mwangela aliishukuru kampuni hiyo na akiwataka wanafunzi kujua
mataifa rafiki yenye nia njema kwa nchi yetu kwa manufa ya vizazi vijavyo.
Mkuu wa Wilaya hiyo aliwataka wananchi kutobwaga manyanga
katikakufanya shughuli za maendeleo wakitegemea kuendelea kupata misaada kama
hiyo,bali mipango waliyojiwekea iendelee kutekelezwa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Mhe. Ubatizo Songa Songa
akizungumza kwa niaba ya wananchi aliwataka wazazi na walezi kufanya vitu
vingine vyenye manufaa kwa elimu baada ya pengo la madawati na vifaa hivyo
vingine kuzibwa kwa msaada huo.
Wanafunzi wa shule hiyo kupitia nyimbo na mashairi waliweza
kuonesha furaha jinsi watakavyoongeza bidii katika masomo na michezo.
Hotuba ya kampuni hiyo ilihimiza umuhimu wa kuwekeza katika elimu ili
kufikia malengo mbalimbali ya kitaifa ambayo yakisimamiwa vema huleta maendeleo
na kulipa taifa heshima mbele ya mataifa mengine.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kakoma Wilayani Ileje mkoa wa Njombe wakifurahia vifaa mbalimbali vilivyokuwa vimewasilishwa hapo shuleni kwao
tayari kwa makabidhiano.
Sehemu ya vifaa vya michezo iliyopokelewa na baadaye vitagawiwa kwa shule za Msingi na Sekondari wilayani
Ileje
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia
Jenerali Nicodemas Mwangela (aliyevaa skafu) akipokea madawati na viti 200 toka
kwa mmoja wa wakilishi wa kampuni ya Kichina ya GEO Company
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...