SERIKALI imeendelea kuboresha huduma za matibabu ya kifua Kikuu kwa kuongeza vituo vya kutolea huduma za matibabu sambamba na kuongeza vifaa tiba, ikiwa ni jitihada za Serikali kutokomeza ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu leo wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za kifua Kikuu na kutoa tamko kuhusiana na ugonjwa huo katika Hospitali ya Mbagala Jijini Dar es salaam.

"Huduma za matibabu ya Kifua Kikuu (TB) sugu zimesogezwa karibu kwa wananchi, ambapo kwa sasa tunazo hospitali 93 za kutibu Kifua Kikuu sugu ikilinganishwa na mwaka 2015 ambapo, huduma za matibabu zilikuwa zinapatikana katika Hospitali ya Kibong'oto pekee " amesema Waziri Ummy.

Pia, Waziri Ummy amesema katika kila Watanzania 100,000 Watanzania 269 wanahisiwa kuwa na ugonjwa wa Kifua Kikuu, huku watu 70 wanafariki kila siku kutokana ugonjwa wa Kifua Kikuu ambapo ni sawa na watu watatu hufariki kila saa.

"watu 70 kila siku kutokana na ugonjwa wa Kifua Kikuu, kwahiyo kila saa ni sawa na watu watatu wanafariki kutokana na ugonjwa wa Kifua Kikuu ambao unatibika " alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema takribani wagonjwa 154,000 wanaokadiriwa kuugua ugonjwa wa Kifua Kikuu wanapaswa kufikiwa na kuingizwa katika mpango wa matibabu kila mwaka ili kuutokomeza ugonjwa huu nchini.

Waziri Ummy ameendelea kusema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi 30 Duniani zenye kiwango kikubwa cha wagonjwa wa Kifua Kikuu, inakadiriwa kuwa wapo wagonjwa takribani 154,000 ambao huugua ugonjwa wa kifua Kikuu kila mwaka.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa Mgonjwa wa Kifua Kikuu ambae hajaanza matibabu anaweza kuambkiza Kati ya watu kumi hadi watu 20 kwa mwaka, hivyo jitihada za makusudi zinatakiwa kuendelea kuchukuliwa ili kutokomeza ugonjwa huu nchini.

"ifahamike kuwa mgonjwa wa kifua Kikuu ambae hajaanza matibabu anaweza kuambukiza kati ya watu kumi hadi watu ishirini kwa mwaka, hivyo tunalojukumu kubwa lakuhakikisha tunawafikia wote wanaougua ili tuweze kuzuia maambukizi mapya ya Kifua Kikuu" alisema Waziri Ummy

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesema kuwa kitaifa tunakadiliwa kuwa wapo wagonjwa wa Kifua Kikuu sugu takribani 200 na kati yao, wagonjwa 167 sawa na 84% walianzishiwa matibabu, huku akitoa wito kwa wagonjwa wengine kujitokeza kupata matibabu.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaviva amemuomba Waziri Ummy kuona ulazima wa kuipanua Hospitali ya Mbagala, ili kurahisisha utoaji huduma za Afya, kwani takribani wanawake 67 mpaka 70 hujifungua kwa siku.

"Wakina mama wanaojifungua hapa ni wengi sana, kwa Mfano jana tu wakina mama 67 wamejifungua, siku nyingine wanafika 70 mpaka 80, hivyo tunahitaji ipanuliwe hospitali hiyo " alisema Mhe. Felix Lyaviva

Nae Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Mbagala Dkt. Dk Ally Mussa amesema kuwa kutokana na maboresho makubwa ya hospitali kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa hadi kufikia wagonjwa 1700 kwa siku, kumekuwa na maboresho makubwa ya huduma za mama na mtoto, maboresho ya huduma za uchunguzi wa magonjwa (maabara za kisasa)

"kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa baada ya maboresho mengi katika huduma za Afya za hospitali, kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa hadi kufikia wagonjwa 1700 kwa siku" alisema Dkt. Dk Ally Mussa.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wa (kushooto) akisema jambo na wananchi wa Mbagala alipotembea Hospitali ya Mbagala Jijini Dar Es Salaam na kutoa tamko la Siku ya Kifua Kikuu duniani.(wapili kushoto),Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akitoa dawa za Kifua Kikuu kwa Bw. Abbas Sudi alipotembelea Hospitali ya Mbagala Jijini Dar Es Salaam kujionea hali ya utoaji huduma za matibabu ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu na kutoa Tamko la Serikali katikabkuadhimisha Siku ya Kifua Kikuu Duniani amnayo huadhimishwa Tarehe 24 Machi kila Mwaka.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akitoa dawa za Kifua Kikuu kwa Bi. Aisha Rashid alipotembelea Hospitali ya Mbagala Jijini Dar Es Salaam kujionea hali ya utoaji huduma za matibabu ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu na kutoa Tamko la Serikali katikabkuadhimisha Siku ya Kifua Kikuu Duniani amnayo huadhimishwa Tarehe 24 Machi kila Mwaka.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akiangalia zawadi ya nguo aliyopewa na Taasisi ya Mukukite inayojishughulisha kutoa huduma za matibabu ya ugonjwa wa kifua kikuu.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Felix Lyaviva akizungumza na wanachi wa Mbagala leo jijini Dar es Salaa ambapo amewaomba wananchi wanapoona dalili za (TB) waende mapema Hospitali watatibuwa bure.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Felix Lyaviva pindi alipofanya ziara na kujionea huduma za matibabu ya ugonjwa wa Kifua Kikuu katika Hospitali ya Mbagala leo jijini Dar Es Salaam.picha zote na (Emmanuel Maasaka,MMG)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wapili kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Felix Lyaviva (wa kwanza kushoto) pamoja na wadau mbalimbali wa afya wakiwasili katika Hospitali ya Mbagala leo jijini Dar Es Salaam.picha zote na (Emmanuel Maasaka,MMG)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa mtaalam kuhusu uchugnguzi wa ugonjwa wa Kifua Kikuu alipotembelea Hospitali ya Mbagala leo jijini Dar Es Salaam.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...