Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MAGOLI matatu ya timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' dhidi ya timu ya Taifa ya Uganda ' The Cranes' yametosha kuwapelekeaWatanzania nchini Misri kwenye michuano ya AFCON mwaka 2019.

Mbele ya mashabiki  zaidi ya 60,000 ambao walikuwa na jukumu la kuhakikisha wanaishangalia Taifa Stars yalikuwa chachu tosha kwa wachezaji ambapo waliokuwa wanacheza kwa uwezo wa hali ya juu.

Taifa Stars ilipata goli la kwanza kupitia kwa Mshambuliaji wake Simon Msuva ambalo liliduma hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza, hadi wanakwenda mapumziko Taifa Stars ilikuwa inaongoza kwa goli 1-0 dhidi ya The Crains.

Wakati wachezaji wa timu ya Taifa Stars wakicheza kwa jihadi huku wakitambua kaulimbiu inayosema ' Ni zamu yetu', kipindi cha pili walirudi uwanjani wakiwa na nguvu zaidi na kufanya mashambulizi ya mara kwa mara golini kwa 'The Cranes'.

Mashambulizi ya Taifa Stars yalisababisha kupatikana kwa penalti kwa upande wa Tanzania ambapo mchezaji aliyekuonesha umahiri wa hali ya juu kumiliki mpira Erasto Nyoni aliifunga goli la pili.

Kasi ya Taifa Stars ilisababisha kupatikana kwa goli la tatu kupitia kwa mchezaji Agrey Morris.

Hata hivyo wachezaji wa Uganda walionekana kusuka mipango ya kutafuta bao lakini Taifa Stars waliziba njia zote na kuharibu mipango na kuifanya kushindwa kupata goli.

Watanzani waliokuwa uwanjani wakiongozwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa walikuwa na furaha isiyo kifani huku wachezaji wa Taifa Stars wakionesha kuwa kichwani wanaiwaza AFCON na sio kitu tofauti na hicho.

Magoli ya Taifa Stars yalisababisha mashabiki kushindwa kukaa kwenye viti ambapo karibu muda wote wa mchezo walikuwa wakishangilia.

Hata hivyo wakati Taifa Stars na Uganda wakiendelea kuchezaji,mashabiki walitangaziwa kuwa mechi kati ya Lesotho na Cape Verde yalikuwa ni sare .Matokeo hayo yameipeleka Taifa Stars na Uganda Misri hasa kwa kuzingatia Uganda walishafuzu kwa kuwa na alama 13 kabla ya mchezo wa leo.



Hata hivyo mashabiki wa Uganda waliokuwa uwanjani hapo walionekana nao wakishangilia ushindi wa Taifa Stars.Kabla ya kuanza kwa mechi ya leo iliyofanyika Uwanja Mkuu wa Taifa mashabiki wa Uganda walikuwa na matumaini ya kushinda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...