Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa,Dk.Gaudentia Kabaka akimkabidhi zawadi ya Saa yenye picha yake Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan (Kulia) katika Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.Picha Zote na Elisa Shunda

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU AWAONGOZA WANAWAKE WA UWT TANZANIA KATIKA KONGAMANO LA KUMPONGEZA RAIS DK.SHEIN KWA KUTIMIZA MIAKA MITATU YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM YA MWAKA 2015/2018 MJINI UNGUJA.

 Pwani Kucheleeeeeeeeeee

  Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa,Dk.Gaudentia Kabaka akiongozana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan (Kulia) katika Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

  Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokea Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakifuatilia kwa umakini wakati Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

 Viongozi Wakiongozwa na Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassan (katikati) wakiimba wimbo wa taifa katika Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.


 Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa,Dk.Gaudentia Kabaka akijadiliana jambo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan (Kulia) katika Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

 Mwenyekiti wa Uwt Mkoa wa Pwani,Farida Mgomi (wa pili kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu Mkuu Uwt Taifa,Mwalimu Queen Mlozi (wa tatu kutoka kushoto) katika kongamano hilo.

  Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokea Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakifuatilia kwa umakini wakati Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

 Viongozi Mbalimbali wa Serikali Mawaziri,Manaibu Mawaziri,Wakuu wa Mikoa na Wilaya na Wakurugenzi toka Sekta Mbalimbali wakifuatilia kwa umakini wakati Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

  Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokea Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakifuatilia kwa umakini wakati Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

  Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokea Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakifuatilia kwa umakini wakati Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

  Mwenyekiti wa Uwt Mkoa wa Pwani,Farida Mgomi (katikati) na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Uwt Wilaya ya Kibaha Mjini,Mwalimu Joyce Francis (kushoto) wakifuatilia kwa umakini wakati Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

 Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) Mkoa wa Pwani,Farida Mgomi akisalimiana na Mwenyekiti wa UWT Taifa, Dk.Gaudentia Kabaka (aliyekaa chini)  katika Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

  Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokea Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakifuatilia kwa umakini wakati Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

 Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokea Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakifuatilia kwa umakini wakati Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 likiendelea katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.

Mwenyekiti wa Uwt Taifa,Dk.Gaudentia Kabaka (kulia) akizungumza kwenye Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana. Kulia ni Makamu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan.

 Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akijadiliana Jambo na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk.Abdallah Juma Mabodi (katikati) na Katibu Mkuu wa Uwt Taifa,Mwalimu Queen Mlozi (Kulia) wakati wa Kongamano hilo likiendelea.

 Mke wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Abeid Amani Karume, Mama Fatuma Karume akitafakari jambo wakati wa Kongamano hilo likiendelea kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar jana.

  Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akihutubia katika Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana. Kulia ni Mwenyekiti wa UWT Taifa,Dk.Gauedentia Kabaka.

 Katibu Mkuu wa UWT Taifa,Mwalimu Queen Mlozi akizungumza katika Kongamano hilo.

Naibu Waziri wa Nishati wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Subira Mgalu,akisalimiana na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ushirikiano uliopo kati ya Shirika la Umeme la Tanesco na Shirika la Umeme la Zanzibar katika kuhakikisha umeme unapatikana na Kuelezea wizaara hiyo inavyotekeleza majukumu yake katika sekta ya Nishati nchini katika Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana. Kushoto ni Mwenyekiti wa UWT Taifa,Dk.Gaudentia Kabaka.

 Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akiagana na Mwenyekiti wa Uwt Taifa,Dk.Gaudentia Kabaka (kulia) baada ya Kongamano la Wanawake Zanzibar la Kumpongeza Rais Dk.Shein kwa Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa miaka 3 kuanzia Mwaka 2015/2018 katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Hotel ya Verde Mjini Unguja Zanzibar Jana.



NA:ELISA SHUNDA,UNGUJA,ZANZIBAR.
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
amesema Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar Dk.Ali
Mohamed Shein ameitendea haki ilani ya uchaguzi wa Chama Cha
Mapinduzi(CCM) ya mwaka 2015/2018 katika kipindi cha miaka mitatu
aliyoongoza Zanzibar.

Pia, amesema utendaji huo umejidhihirisha katika jitihada zake za
kuendeleza na kuimarisha kwa ufanisi mkubwa azma ya machi 3 mwaka 1965
ya Rais wa kwanza wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hayati Abeid
Aman Karume ya kutoa huduma za matibabu bure kwa wananchi.

Kauli hiyo ameitoa jana katika kongamano la wanawake la kumpongeza
Rais Dk.Ali Mohamed Shein kwa kutimiza miaka mitatu ya utekelezaji wa
ilani ya uchaguzi ya CCM iliofanyika mjini Unguja liloandaliwa na
Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT) ya Chama cha CCM.

Makamu huyo wa Rais alisema katika uongozi wa Rais Dk.Shein
ametekeleza zaidi katika azma hiyo kwa kuhakikisha anaongeza bajeti ya
dawa kwa kila mwaka ambapo kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ametenga
sh.bilioni 12.7 huku akiongeza watumishi wa afya pamoja na upatikanaji
wa vifaa tiba vya kisasa.

"Huduma hizi zimeendelea kuboreshwa zaidi hususan kwa wazee nampongeza
kwa hatua ya kuwapatia vitambulishi 2,314 wazee kwa lengo la kuwapatia
pensheni ili kuhakikisha wanapata huduma za matibabu bure,"alisema
Makamau huyo wa Rais

Katika maelezo yake Samia alisema wanzanzibar ni mashahidia wa namna
utekelezaji wa ilani ambao Dk.Shein ameufanya kwa kiwango cha juu
ambapo shule za maandalizi zimeongezeka kwa mara 272 baada ya kipindi
cha mapinduzi.

Alisema kwa upande wa shule za msingi zimeongezeka mara 7 huku kwa
sekondari zikiongezeka kwa mara 67 na kwamba katika kipindi cha miaka
mitatu mbali na kuboresha miundombinu ya elimu ikiwemo
madarasa,maabara na matundu ya vyoo.

"Pia Rais Dk.Shein amewaondolea wazazi na walezi mzigo wa kuchangia
elimu ya msingi mwaka 2016 na ya sekondari mwaka 2018 na hatua hii
itasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza mahudhurio na kuondoa ujinga na
kuongeza idadi ya watu walioelimika,"alisema

Makamu huyo wa Rais alisema katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya
CCM Dk.Shein ameendelea kuwajali watu wa iana zote bila ya ubaguzi
ambapo wazee ambao wamefikisha miaka 70 na kuendelea wanapewa fedha za
kujikimu ya sh.20,000 kwa kila mwezi.

"Kwa upande wa sekta ya uvuvi ambayo bado hatujaitumia ipasavyo kwa
dhati jitihada za kutengeneza meli mbili ambazo zitakuwa na uwezo wa
kuhifadhi tani 86 za samaki kwa kipindi cha wiki mbili wakiwa baharini
pamoja na mapitio ya sheria ya vyama vya ushirika na uandaaji wa mfumo
wa kietroniki wa kukusanya,kuchambua na kutoa takwimu za vyama vya
ushirika vitaleta matokeo chanya,"alisema Makamu huyo wa Rais

Samia aliongeza kuwa anampongeza Rais Dk.Shein kuendelea na jitihada
zake za kutoa ruzuku kwa wakulima hususan kwa zao la mpunga na kwamba
zimeongeza uzalishaji na kuongeza kipato kwa wananchi na mapato kwa
serikali ya SMZ.

"Pia nampongeza kwa kuendeleea kuhakikisha kuwa zao letu la karafuu
linasimamiwa vizuri na wananchi wanafaidika na kilimo hichi na wazo la
kuanzisha Taasisi ya utafiti wa mifugo na kwamba wazo hili limekuja
kwa wakati kipindi ambacho tayari kiwanda kikubwa cha kuzalisha maziwa
kimeshafunguliwa Zanzibar,"alisema

Makamu huyo wa Rais aliongeza kuwa Dk.Shein ameendelea kutendea haki
katika utekelezaji wa ilani kwa upande wa ujenzi wa viwanja vya ndege
ambapo ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa Abeid Karume mjini Unguja
unaendelea kutekelezwa na uwanja wa ndege wa Pemba unatarajia kuanza
ujenzi wake hivi karibuni.

Hata hivyo, Samia aliwataka wanawake visiwani humu kuchukua jukumu la
kuzisemea na kuzitangaza kwa sauti kazi kubwa nzuri zinazofanywa na
viongozi wa serikali mbili ili wananchi wazijue na wasipotoshwe.

Kwa upande wa Mwenyekiti Taifa wa Jumuiya ya Umoja wa
Wanawake(UWT),Gaudencia Kabaka alisema katika kipindi cha hivi
karibuni jumuiya hiyo imefanya ziara kwa upande wa Unguja na Pemba kwa
ajili ya kuelezea namna CCM ilivyotekeleza ilani yake.

Alisema kwa asilimia kubwa CCM imetekeleza ilani yake visiwani humu
ambapo hali hiyo inatokana na ushirikiano mkubwa na wa karibu uliopo
kati ya serikali ya SMZ na CCM.

"Nimejifunza mambo mengi hasa nilipofika kwenye ziara zangu ikiwemo
ushirikiano mkubwa ulioko kati ya Serikali ya SMZ na chama na kwamba
kila tulipoenda tulikutana na watendaji wa serikali ambao ndio
watekelezaji wa ilani huku wakitueleza mambo yalivyotekelezwa,"alisema

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa UWT,Queen Mlozi alisema jumuiya hiyo
itaendelea kushirikiana na viongozi wa CCM ambao kwa kiasi kikubwa
wameendelea kutekeleza vyema ilani ya uchaguzi wa CCM.

Alisema kupitia viongozi hao wameendelea kuwapatia wanawake nafasi
mbalimbali za uongozi ikiwemo nafasi za Uwakilishi,Ubunge na katika
ngazi za serikali za SMZ na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.

"Kwa mfano Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi ni mwanamke na Naibu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ni mwanamke nataka niseme na
hiyo inatokana na kujitambua na kujiamini kwetu hivyo tupo bega kwa
bega kuhakikisha CCM inaendelea kuongoza kwa upande wa Zanzibar na
Tanzania,"alisema

Akizungumza kwa niaba ya Uwt Mkoa wa Pwani,Farida Mgomi,alimpongeza Rais Shein kwa utekelezaji mzuri wa Ilani ya CCM katika miaka 3 tokea 2015 hadi 2018 kupitia mawaziri wake waliowasilisha maelezo ya utendaji kutoka kwenye wizara zao na amemshukuru katibu mkuu wa Uwt Taifa,Queen Mlozi kwa mwaliko na amewakumbusha viongozi wenzake ngazi ya mkoa na wilaya kuandaa makongamano katika ngazi zao kuisemea serikali yao kwa utekelezaji mzuri wa ilani ya CCM kwa wananchi na wanachama wa chama hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...