Leo tarehe 21 mwezi March katika elimu ya Jiografia ni kwamba Jua lipo katika mstari wa Ikweta ambao unaigawa dunia katika sehemu mbili yaani hemispheres kwa maana ya upande wa Kaskazini na Kusini ... Northern Hemisphere and  Southern hemispheres . Kwa maana hiyo leo tarehe 21 mwezi Machi na tarehe 23 mwezi September jua linakuwa katika mstari wa Ikweta ambao unaigawa dunia katika sehemu mbili yaani Kaskazini na Kusini.
Hivyo leo sehemu zote duniani urefu wa mchana na usiku unalingana. Yaani kwa maana nyingine sehemu zote duniani zinapata urefu sawa wa mchana na usiku. Hali hii kijiografia inajulikana kama Equinox yaani maana yake equal night and equal day.

Hii inamaanisha nyakati zingine zote ukitoa hizi siku mbili yaani tarehe 21 Machi na 23 Septemba urefu wa usiku na mchana hutofautiana.  Nakutakia siku njema ya "Equinox" ambayo sehemu zote duniani urefu wa usiku na mchana unalingana. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...