Na Sultani Kipingo
Aghalabu ndege inapopata dharura angani,
waongoza ndege waliopo ardhini hawasiti kuiruhusu kurudi uwanjani, wakati
mwingine kutokana na kusahaulika kitu. Majuzi kati katika uwanja wa Mflamu
Abdulazizi wa Saudi Arabia mama mmoja alisahau motto wake mchanga hapo
uwanjani.
Yaani huyo mama, aliyekuwa anasafiri na ndege
ya Shirika la Ndege la Saudi Arabia, alisahau kichanga chake kwenye eneo la
kusubiria la wanaoondoka. Kwa mujibu wa gazeti la Gulf News, japokuwa yeye ni
mzazi, mama huyo alipanda hiyo ndege akiwa hana shaka na jambo lolote.
Ni wakati ndege ikiwa imeshapaa angani ndipo
akakumbuka kwamba kaacha kichanga uwanjani! Na mara tu baada ya kugundua hilo,
akawaarifu wahudumu wa ndege kwamba kasahau motto mchanga uwanjani, na kumfanya
rubani wa Ndege namba SV832 kutoka mji mkuu wa Saudi Arabi, Jeddah, ikielekea Kuala
Lumpur, Malaysia, irudi uwanjani.
Tukio hilo lilishangaza kila mtu wakiwemo
wahudumu wa ndege, abiria wenzake na hata waongoza ndege uwanjani Jeddah. Video
inayoonesha rubani wa ndege hiyo akiomba ruhusa kurudi uwanjani kumchukua motto
mchanga aliyesahaulika imeshika kazi mitandaoni huku wengi wakijiuliza mtu
unasahau vipi motto wako?
“Ndege hii inaomba ruhusa kurudi…kuna abiria
kasahau kichanga chake uwanjani, maskini”, rubani anasikika katika video hiyo.
Waongoza ndege walichukua dakika kadhaa
kufikiria itifaki ipi itumike katika kuruhusu ndege kurejea uwanjani kwa sababu
kama hiyo.
“Haya rudi tena getini. Hili ni jambo jipya
kwetu!” anasema mmoja wa waongoza ndege. Hata hivyo ndege ikatua na mama
akaungana na kichanga chake na kuendelea na safari baadaye.
The ATC
executives spent several minutes figuring out the protocol to be observed
during such incidents. “Ok, head back to the gate. This is totally a new one
for us!” says one of the ATC operator. The woman was finally reunited with her
baby at the airport.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...