Serikali ya Marekani ilikabidhi vifaa vya kupimia maji kwa Bodi za Mabonde ya Maji Rufiji na Wami / Ruvu. Vifaa na huduma za ziada vitasaidia bodi kukusanya na kuchambua takwimu juu ya ubora na kiasi cha maji. Ufuatiliaji wa uboreshaji wa maji utasaidia wilaya kufanya maamuzi sahihi juu ya ugawaji wa maji ili kusimamia na kulinda rasilimali za maji kwa vizazi vijavyo.

Mbali na vifaa vya kupimia maji, Bodi za Maji zilipata boti/mashua, kompyuta, redio, vifaa vya kukadiria umbali, na vifaa vya mtandao kwa shughuli za zinazofanyika katika eneo la mradi na ofisini. Wafanyakazi watafundishwa namna ya kutumia vifaa vya kupimia maji ya mtoni.

Vifaa na huduma, vyenye thamani ya shilingi bilioni 2.3 za Kitanzania (dola 980,000 za Kimarekani), zilikabidhiwa na Shirika la WARIDI, na kufadhiliwa na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID). WARIDI inaendeleza usimamizi wa rasilimali maji na kuboresha upatikanaji wa huduma za maji.

“Kwa sababu maji yana jukumu muhimu katika kupunguza umasikini, kuboresha afya, na kuongeza uzalishaji, ni lazima yapewe kipaumbele cha juu serikalini na jumuiya ya wafadhili,” alisema Andrew Karas, Kaimu Naibu Balozi wa Ubalozi wa Marekani.

Kupitia WARIDI, Serikali ya Marekani pia ilipatia Wizara ya Maji mwongozo wa matumizi ya kutathmini uwezo wa Jumuiya za Watumia Maji (WUAs), asasi za kijamii zinazohusika na usimamizi wa rasilimali za maji. WUA wana mamlaka ya kisheria ya kupata na kutumia vibali vya matumizi ya maji, kutatua migogoro ya matumizi ya maji, kulinda vyanzo vya maji, kuwakilisha maslahi ya watumiaji katika ngazi ya jamii, na kukusanya tozo za watumiaji wa maji kwa niaba ya Bodi za Mabonde za Maji.
 

 Kifaa kinaweza kutumika kwa ufuatiliaji wa mara kwa mara wa WUA na kutambua hatua za kuboresha utendaji. Ilianzishwa kupitia mchakato shirikishi unaohusisha wawakilishi kutoka Bodi ya Maji ya Bonde, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Wizara ya Maji, na washauri wa ndani.

Ili kuomba taarifa zaidi, tafadhali piga simu Ofisi ya Habari ya Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam kupitia: +255 22 229-4000 au barua pepe: DPO@state.gov.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...