Jeshi la Polisi nchini limeelekezwa kutumia wafungwa ili kuweza kuokoa kiasi cha Shilingi Milioni Mia Mbili kati ya Milioni Mia Saba zilizotolewa na Rais Dk. John Magufuli katika Mradi wa Ujenzi wa Mabweni na Madarasa ya Chuo cha Taaluma ya Polisi kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam.
Maelekezo hayo yametolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni alipotembelea majengo chakavu ya chuo hicho baada ya kupokea kiasi cha Shilingi Milioni Mia Saba alizoahidi Rais Dkt. John Magufuli akihutubia katika mahafali ya kuhitimisha Mafunzo ya Kozi za Uofisa na Ukaguzi Msaidizi chuoni hapo mwishoni mwa mwaka jana
“Wizara ina taasisi ya magereza ambayo ina nguvu kazi ya kutosha, na Rais alishaagiza wafungwa watumike katika shughuli za uzalishaji, sioni sababu ya kutumia kiasi hicho cha pesa kuwalipa vibarua wa nje, naagiza muwasiliane na Jeshi la Magereza pamoja na kikosi cha ufundi kilichopo ndani ya Jeshi la Polisi ili muweze kuona ni vipi mnaokoa kiasi hicho”alisema Masauni
Akitoa taarifa ya awali ya ujenzi huo, Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi, Naibu Kamishna Anthony Rutashuburugukwa alitaja majengo yatakayojengwa kuwa ni ghala la chuo, madarasa matatu,bweni moja la askari wa kiume na bweni lingine la askari wa kike.
Wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa majina wanafunzi wa chuo hicho walimshukuru Rais Dkt. Johh Magufuli kwa kiasi cha fedha alichotoa ili kuweza kujenga sehemu mbalimbali za chuo hicho ikiwemo mabweni ambayo wamekiri ni chakavu na si rafiki kwa matumizi ya binadamu.
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza
na Askari Polisi ambao ni wanafunzi katika Chuo cha Taaluma ya
Jeshi la Polisi, wakati alipotembelea chuoni hapo kufuatilia
maandalizi ya awali baada ya jeshi hilo kupokea kiasi cha Shilingi
Milioni Mia Saba kutoka kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa ajili ya ujenzi
wa chuo hicho.Ziara hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam. Picha
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akitembelea
maeneo ya Chuo cha Taaluma ya Polisi ambacho hivi karibuni kimepokea
Shilingi Milioni Mia Saba kutoka kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa ajili
ya ujenzi wa majengo ya chuo hicho, kulia ni Mkuu wa Chuo, Naibu
Kamishna, Anthony Rutashuburugukwa. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati),
akitembelea maeneo ya Chuo cha Taaluma ya Polisi ambacho hivi karibuni
kimepokea Shilingi Milioni Mia Saba kutoka kwa Rais Dkt. John Magufuli
kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya chuo hicho,Wengine ni viongozi
wa chuo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisalimiana
na Maafisa wa Jeshi la Polisi wakati wa ziara katika Chuo cha Taaluma
ya Polisi, jijini Dar es Salaam ambacho hivi karibuni kimepokea
Shilingi Milioni Mia Saba kutoka kwa Rais Dkt. John Magufuli kwa ajili
ya ujenzi wa majengo ya chuo hicho. Picha na Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...