Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MOTO umewaka CUF!Ndio maneno unayoweza kuelezea mgogoro unaondelea ndani ya Chama cha Wananchi(CUF) ambapo imefikia hatua ya kufuta rangi ya chama hicho katika vijiwe vya matawi na kupaka rangi ya ACT-Wazalendo.

Kufutwa kwa rangi ya CUF kwenye mashina hayo kuna baada ya Mahakama kutoa uamuzi unamtambua Profesa Ibrahim Lupumba kama Mwenyekiti halali wa Chama hicho.

Baadhi ya mashina ya CUF ambayo yameonekana yakifutwa ni yale yaliyokuwa visiwani Pemba katika tawi la Jows Corner Stone Town ambapo baadhi ya wanachama wameamua kufuta rangi ya CUF na kukapa rangi ya bendera ya ACT-Wazalendo.

Hata hivyo inaelezwa kuna tetesi zinazodai huenda Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akahamia Chama cha ACT-Wazalendo ambacho kiongozi wake ni Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe.

Michuzi Blog itaendelea kukupa taarifa zaidi ya kinachoendelea ndani ya CUF kwa sasa...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...