Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
MOTO
umewaka CUF!Ndio maneno unayoweza kuelezea mgogoro unaondelea ndani ya
Chama cha Wananchi(CUF) ambapo imefikia hatua ya kufuta rangi ya chama
hicho katika vijiwe vya matawi na kupaka rangi ya ACT-Wazalendo.
Kufutwa
kwa rangi ya CUF kwenye mashina hayo kuna baada ya Mahakama kutoa
uamuzi unamtambua Profesa Ibrahim Lupumba kama Mwenyekiti halali wa
Chama hicho.
Baadhi ya mashina ya CUF ambayo yameonekana yakifutwa ni yale yaliyokuwa visiwani Pemba katika
tawi la Jows Corner Stone Town ambapo baadhi ya wanachama wameamua
kufuta rangi ya CUF na kukapa rangi ya bendera ya ACT-Wazalendo.
Hata
hivyo inaelezwa kuna tetesi zinazodai huenda Katibu Mkuu wa CUF Maalim
Seif Sharif Hamad akahamia Chama cha ACT-Wazalendo ambacho kiongozi wake
ni Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe.
Michuzi Blog itaendelea kukupa taarifa zaidi ya kinachoendelea ndani ya CUF kwa sasa...
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...