Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Freeman Mbowe amesema Chama cha Wananchi(CUF)kinapita katika wakati mgumu kutokana na mgogoro unaondelea kufukuta ndani ya Chama hicho.

Mbowe amesema hayo leo Machi 15,2019 jijini Dar es Salaam wakati anazungumza na waandishi wa habari ambapo amedai mgogoro wa CUF umetengeneza kwa lengo la kuudhoofisha upinzani.

"CUF inapita kwenye mgogoro mkubwa na kwa bahati mbaya ni wa kutengenezwa kwa lengo la kuudhofisha upinzani.Sitaki kuwa Msemaji wa CUF ila nawashauri wamalize kile ambacho watakifanya kwa usalama,"amesema Mbowe.

Ameongeza wakati mgogoro huo unaendelea, amemsikia mara kadhaa Profesa Ibrahim Lipumba namna ambavyo anawalaumu Chadema na uamuzi wake wa kujiondoa Ukawa.

"Profesa Lipumba ni mtu ambaye nimefanya naye nyingi, naheshimu na nitaendelea kumheshimu.Kwa sasa nimuache maana ni mtu mzima na acha afanye anachoendelea.

"Kuna siku Dunia itajua na hasa muda ukifika utaongea.Naamini haki ya wananchi wa Zanzibar kupiria maalim Seif Sharif Hamadi na Chama chake itapatikana tu.Nimuombee mema Maalim Seif na watambue haya ni mapito tu na watayapita, "amesema.

Prof Lipumba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...