Mstahiki Meya Manispaa ya Ubungo Mh,Boniface Jacob leo amegawa vyerehani kumi (10), Vya kisasa Vinavyogharimu kiasi cha Tsh Millioni 20 Kwa Vikundi viwili (2) Vya Wanawake Manispaa ya Ubungo ambavyo ni MASHUJAA WOMEN GROUP na VICTORIA FOUNDATION GROUP

Katika Hafla hiyo ya ugawaji wa Misaada hiyo ya vyerehani kumi (10),lengo kubwa ikiwa ni Kuwawezesha Wanawake kujikwamua kiuchumi, na kuwapatia Mafunzo ya ushonaji na Ujasiriamali 

Mstahiki Meya ameshirikiana na Kiwanda Cha Ushonaji cha SPESHOZ TANZANIA ambapo Mkurugenzi wake Bw,Jeffrey Jessey amesema Kampuni Yake Itaunga mkono Juhudi za Mstahiki Meya za Kuwawezesha Wanamke kujikwamua Kiuchumi kwa Kutoa Mafunzo ya Miezi mitatu(3) kwa wanawake 48 wa Vikundi vyote viwili Vya wakina Mama Waliopokea Misaada hiyo Kwa awamu hii ya Kwanza.

Aidha Mkurugenzi mwenza wa SPESHOZ TANZANIA Bi Cecilia Mosha, ameahidi kuendelea kutoa Ushirikiano Kwa Mstahiki Meya katika awamu zingine zitakazo fuatia Katika Programu ya Ugawaji Vyerehani kwa ajili ya Kumsaidia Mwanamke Kujikwamua Kiuchumi, Pamoja na kutoa wito kwa Wanawake wengine kuitikia fursa ya Mstahiki Meya na kufanyia kazi kwa Vitendo kauli ya Rais Magufuli ya Tanzania ya Viwanda

Mstahiki Meya ametoa wito kwa wakina Mama wengine ndani ya Manispaa ya Ubungo kuendelea kuandika barua za Maombi na Maandiko ya Mchanganuo ya Miradi ya Ushaonaji ,Kwa ajili ya kupatiwa Misaada Awamu zingine zinazofuata.
Mstahiki Meya Manispaa ya Ubungo Mh,Boniface Jacob (katikati) akiwakabidhi vyerehani kumi vikundi viwili vya wajasiriamali wanawake vyenye thamani ya Millioni 20 leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Maasaka,MMG)
Mstahiki Meya Manispaa ya Ubungo Mh,Boniface Jacob (katikati) akizungumza leo jijini Dar es Saam katika hafla ya ugawaji ya vyerehani kumi vyenye thamani ya Millioni 20 kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...