Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Mohamed Kambi ameiomba Serikali ya Uarabuni kundelea kutoa misaada mbalimbali ukiwamo wa kujenga hospitali kubwa nchini ili kuwasaidia wagonjwa mbalimbali nchini. 
Kauli hiyo imetolewa na Prof. Kambi wakati akifungua mafunzo ya siku mbili yalioandaliwa na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na Al balsam Cure and Care International Charity Organization kwa ajili ya kuwawezesha wataalam wa afya kusimamia upumuaji kwa wagonjwa waliolazwa ICU.
“Natambua kwamba Serikali ya Uarabuni imekuwa ikitoa misaada mingi ya kuboresha huduma za afya, hivyo naomba wajenge hospitali kubwa nchini kwa ajili ya kutoa huduma za afya nchini,” amesema Prof. Kambi.
Prof. Kambi amewataka wataalam wanaopata mafunzo hayo kuyatumia vizuri katika sehemu za kazi pamoja na kuwaelimisha wataalam wengine.
Pia, Mganga mkuu ameishukuru Serikali ya Uarabuni kwa msaada wa matibabu ambao wamekuwa wakitoa kwa hospitali mbalimbali nchini ikiwamo Muhimbili na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
Naye Mkurugenzi Rasilimali Watu na Utawala wa Muhimbili, Bw. Makwaia Makani amesema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka kwa kuwa MNH imepanua huhuduma za vyumba vya kulaza wagongonjwa wanaohitaji uangalizi maalamu pamoja na kununua vifaatiba.
Leo, watalaam walikuwa wakifundishwa jinsi vifaa tiba vya ICU vinavyopunguza maumivu kwa mgonjwa na jinsi kudhibiti hewa wakati mgonjwa akipatiwa matibabu ICU. Mafunzo hayo yanawashirikisha wataalam kutoka Hospitali ya Muhimbili, Mbeya, Hospitali ya Benjamini Mkapa, Bugando, Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
 Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Mohamed Kambi akizungumza kwenye mafunzo ya  kuwawezesha wataalam wa afya kusimamia upumuaji kwa wagonjwa waliolazwa ICU. Mafunzo hayo yanafanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
 Baadhi ya washiriki wakimsikiliza Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Mohamed Kambi wakati akifungua mafunzo hayo.
 Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Muhimbili, Bw. Makwaia Makani akizungumza leo kwenye mkutano huo. Bw. Makani alimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Prof. Lawrence Museru.
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Homoni katika hospitali hiyo, Dkt. Faraja Chiwanga akizungumzia umuhimu wa mafunzo hayo kwa wataalam wa ICU nchini.
 
Wataalam kutoka Hospitali ya Bugando, Hospitali ya Benjamini Dodoma, Mbeya na Hospitali ya Mkoa wa Dodoma wakifuatilia mafunzo hayo
 Bw. Alaa Almqatieb akitoa mafunzo kwa  wataalam mbalimbali wa hapa nchini wakiwemo washiriki kutoka Hospitali ya Bugando, Hospitali ya Benjamini Dodoma, Mbeya na Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
 Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Mohamed Kambi akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa afya pamoja wataalam wengine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...