NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 
TIMU ya kitaifa ya kufuatilia na kutatua migogoro ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi wakiwemo wakulima, imeingilia kati mgogoro uliodumu kwa miaka saba baina ya wakulima na wafugaji wa Kwala,wilayani Kibaha Mkoani Pwani na kufanikiwa kuumaliza .

Mgogoro huo unabaki historia baada ya wafugaji wa bonde la mto Ruvu  ,Mwembe Ngozi kupewa agizo la kuondoka na kuhamia eneo la Waya,  ranchi ya Taifa NARCO iliyopo Ruvu ili kuwaacha huru wakulima ambao walikuwa wakipata hasara kutokana na mazao yao kulishiwa mifugo.  

Mkurugenzi msaidizi wizara ya mifugo na uvuvi, ambae pia ni mwenyekiti wa timu hiyo, Dr. Martin Ruheta, aliwataka wafugaji hao akiwemo Sauti Mbili na Masanja Kidirgo ambao wana ng'ombe zaidi ya 500 waondoke kuanzia march 18 mwaka huu. 
Aliwaomba, wafugaji hao na wengine waondoke huku serikali ikiendelea kutafuta maeneo ya kudumu, kwa wale ambao mifugo haitoenea kwenye ranchi hiyo. 

"Timu hii ilianza kazi mwezi octoba mwaka jana, mkoa wa Kigoma, Katavi, Rukwa, Mbeya ambapo kwa mkoa wa Pwani walianzia Mkuranga, Rufiji, Kisarawe na Leo tunamaliza mgogoro huu hapa Kwala "alifafanua Ruheta. 

Nae mkuu wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama alibainisha ,kwasasa hawaombi tena, bali kuanzia jumatatu ijayo waondoke na atakaekaidi akikutwa ng'ombe wake atakuwa halali kwake .

Assumpter aliyaasa, makundi hayo yaheshimiane ili kuondoa migogoro isiyo ya lazima. 

Makamu mwenyekiti wa Chama Cha Wafugaji (CCWT) Esta Moreto alisema ameridhishwa na maagizo hayo ila anaomba wafugaji waondoe mifugo na sio makazi yao kwakuwa wengine wana wanawake wajawazito na watoto. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...