Na Khadija Seif, Globu ya jamii

MCHEKESHAJI chipukizi visiwani  Zanzibar, Abdulnadhif Shaka Hassan ‘Dullyzo’, ametoa ujumbe kwa vijana ambao wanataka mafanikio ya haraka.

Akizungumza leo Dullyzo amesema umaarufu na mafanikio alioyapata hayakuja kimiujiza kwani aliamini ndoto zake pamoja na kujishugulisha na kazi mbalimbali za kijamii.

"Kabla sijawa mchekeshaji nilikua nacheza ngoma na ndio kilikuwa kipaji changu ambacho kilikua kinaniingiza fedha za kujikimu kiuchumi na kuendesha familia," amesema

Hata hivyo ameeleza nini kilimvutia na kuingia kwenye tasnia ya vicheko huku akimtaja Dullivan kama mtu anayefata nyayo zake katika kazi.

“Wakati naanza kumuiga Dullvani, nilitamani siku nikutane naye ili anifundishe baadhi ya njia anazotumia na nashukuru Mungu tumeweza kuonana katika tamasha lililofanyika siku chache zilizopita lililoandaliwa na Zanzibarglamr la mavazi na vipodozi visiwani Zanzibar," amesema Dullyzo

 Amewaasa vijana wa visiwani humo kuchakarika na kujihusisha na kazi yoyote ile ya hali ili kujikwamua kiuchumi na kujiepusha na vitendo viovu vinavyoiathiri jamii kiujumla kama ubakaji,uporaji na uhalifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...