Mkuu wa mkoa wa Katavi Amos Makala katikati akiwa na Mkuu wa wilaya ya Mlele Rachel Kasanda, Dk Theresia Olemako kutoka taasisi ya Jane Godall, , akifuatiwa na Mkuu wa hifadhi ya Katavi Stephano Msumi na kaimu katibu tawala mkoa wa Katavi Awaryiwa Nnko pamoja na watendajiwengine wa mkoa huo.

Mkuu wa mkoa wa Katavi Amos Makala akisoma moja ya bango linaloielezea mbuga ya wanyama ya Katavi.

Baadhi ya picha zikionyesha baadhi ya wanyama wanaopatikana katika mbuga ya wanyama wa Katavi mkoani Katavi.
Mkoa Wa Katavi Umezindua Rasimu Ya Mpango Mkakati Wa Miaka Kumi Ya Kukuza Sekta Ya Utalii Mkoani Katavi Kwa Lengo La Kuongeza Watalii Kutoka Wastani Wa Watalii 3340 Waliotembelea Hifadhi Hiyo Mwaka 2018 Hadi Kufikia Watalii 6012 Mwaka 2029

Akizungumza Mara Baada Ya Kuzindua Rasimu Hiyo Bwana Makalla Amesema Mpango Huo Utawezesha Kukuza Uchumi Wa Mkoa Wa Katavi

Aidha Mkuu Huyo Wa Mkoa Wa Katavi Amewataka Wananchi Kuacha Tabia Ya Kuharibu Mazingira Ili Kuwa Na Maeneo Ya Wanyama Pori Sanjari Na Kuwataka Waandishi Wa Habari Kutumia Taaluma Yao Katika Kuutangaza Utalii Katika Mkoa Wa Katavi Kwani Ni Mkoa Wenye Vivutio Vya Kipekee

Awali Akitoa Taarifa Ya Hifadhi Ya Taifa Ya Katavi Mkuu Wa Hifadhi Hiyo Bwana Stephano Msumi Amesema Wamefanikiwa Kudhibiti Ujangili Wa Tembo Kwa Asilimia Mia Moja Ambapo Kwa Mwaka Uliopita Hakuna Tembo Hata Mmoja Aliyeuwawa

Katika Uzinduzi Huo Kaimu Mtendaji Mkuu Wa Taasisi Ya Jane Goodall Dk. Theresia Olemako Alipata Nafasi Ya Kuwasilisha Mada Juu Ya Wanyama Aina Ya Sokwe Mtu Na Kusema Mwaka 1900 Kulikuwa Na Sokwe Mtu Zaidi Ya Milioni Mbili Lakini Sasa Wamebaki Sokwe Laki Tatu Tu

Mkuu Huyo Wa Mkoa Aliambatana Na Baadhi Ya Wajumbe Wa Kamati Ya Ulinzi Na Usalama Pamoja Na Watendaji Mbalimbali Ambao Walipata Fursa Ya Kutembelea Hifadhi Ya Katavi; Ambapo Walipata Nafasi Ya Kujifunza Namna Mzimu Wa Katabi Unavyoaminiwa Na Watu Wa Jamii Ya Wabende Na Wapimbwe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...