Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha elimu DUCE Chang'ombe jijini Dar es salaam Profesa Bernadeta Killian akipiga mpira wa penati kuashiria ufunguzi wa bonanza la mazoezi ya wafanyakazi wa chuo hicho jana kwenye viwanja vya chuo hicho jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha elimu DUCE Chang'ombe jijini Dar es salaam Profesa Bernadeta Killian akizungumza na wafanyakazi wa chuo hicho wakati akifungua bonanza la mazoezi na michezo kwa wafanyakazi lililofanyika jana chuoni hapo jana jijini Dar es salaam na kushirikisha michezo mbalimbali ikiwemo Mpira wa Miguu, Pete, Bao na Drafti.

Lengo la Bonanza hilo la mazoezi ni kuwafanya wafanyakazi kujiweka sawa kwa afya ya miili yao ili kuwa tayari kutumikia chuo hicho kwa wakiwa na afya na miili iliyo yimamu kabisa kiafya.
Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Bonanza Dk. Julius Mgunai, Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu DUCE Chang'ombe , Naibu Mkuu wa Chuo Kikuu Kishirki cha Elimu DUCE Taaluma Dk. Julius Mbuna na Naibu Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu DUCE Fedha Dk. Method Samwel wakielekea mahali ambapo bonanza hilo lilizinduliwa kwa kupigwa mpira wa penati na Mkuu wa Chuo hicho Profesa Bernadeta Killian.
Naibu Mkuu wa Chuo Fedha Dk. Method Samwel akiwa ameanguka chini baada ya kushindwa kudaka penati iliyopigwa na Mkuu wa Chuo hicho Profesa Bernadeta Killian wakati wa uzinduzi wa bonanza la mazoezi chuoni hapo jana.
Vikosi vya timu zilizoshiriki katika bonanza hilo vikiwa katika picha ya pamoja.
Vikosi vya timu za mpira wa pete vikiwa katika picha ya pamoja.
Wachezaji wa mpira wa miguu wakichuana vikali wakati wa mchezo wa mpira wa miguu.
Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha elimu DUCE Chang'ombe jijini Dar es salaam Profesa Bernadeta Killian akifurahia jambo kabla ya kupiga mpira wa penati wakati wa uzinduzi wa bonanza hilo.
Baadhi ya wafanyakazi wakifurahia mara baada ya hotuba fuoi ya mkuu wa chuo hicho Profesa Bernadeta Killian.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...