NA MWAMVUA MWINYI, MLANDIZI.

MSAFARA wa Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo umezuiliwa na watumiaji wa Stendi ,wafanyabishara wa soko na wauza mitumba (WARUMBA) eneo la Mtongani Mlandizi ,wilayani Kibaha kupinga kuhamia kwenye eneo jipya la Mama Salmini ambako wanadai hakuna maslahi kwao. 

Kufuatia hali hiyo ametoa maelekezo kuwa kutokana na soko hilo kutokuwa mali ya serikali ni ya mtu binafsi kwa maslahi mapana ya wananchi soko la mama salmini wawe huru na wale wanaotegemea Mlandizi waendelee huku wakisubiri ukamilishaji wa soko jipya. 

Kuhusu stendi ,Jafo amesema medereva daladala wanapata shida na stendi wawe na uhuru chini ya usimamizi wa wilaya waendelee kutumia stendi ya mlandizi hadi hapo stendi itakapokmilika. 

Akizingumza na wafanyabiashara hao, alieleza wafanyabiashara hao waachiwe wafenye biashara kwa utaratibu na kufuata sheria bila kubughudhiwa. 

"Nimeangalia idadi ya watu na eneo hilo la mama Salmini wenye hiari ya kufanya biashara wafanye biashara kwenye eneo hilo,lakini na wanaotegemea biashara Mlandizi waendelee "alisisitiza Jafo. 
"Mnajengewa soko la kisasa na serikali ipo kwenye mchakato wa kujengwa stendi mpya,hivyo taratibu nyingine zitafuata. "

Hata hivyo, Jafo alifafanua, Watu wadogo wasinyanyasike ofisi ya mkuu wa wilaya na halmashauri iangalie utaratibu wa kuwasogeza kwenye eneo lisilo hatarishi na wafanya biashara wafuate utaratibu, sheria na utaratibu hadi hapo soko maalum litakapokamilika. 

"Wafanyabiashara toeni ushirikiano na serikali ya chama cha mapinduzi kwa maslahi ya wilaya na mkoa. "alisema Jafo. Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa,aliwataka wawe watulivu na kutoa ushirikiano kwa serikali. Kwa upande wake mwenyekiti wa Warumba ,Nasoro Soma alisema kuwa wao hawako tayari kwenda kufanyabiashara kwenye soko jipya kutokana na mazingira yake hayako vizuri kibiashara .

Alieleza, eneo wanalopelekwa ni dogo na siyo rafiki kufanyia biashara na Halmashauri ikisema sehemu wanayofanyia si sahihi kwani ni barabarani.

Alisema zaidi ya wafanyabiashara 200 wamepata vitambulisho vya ujasiriamali ili kuweza kutambulika.
 Waziri Jafo akizungumza na Wananchi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...