Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akionyesha juu kitabu cha I
Can, I Must, I Will kama ishara ya kuzindua toleo maalum kwa wasioona
(kiatu cha nukta nundu) leo wakati wa hafla ya utoaji tuza ya I CAN
pamoja na chakula cha mchana iliyoandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald
Mengi Persons with Disabilities Foundation katika ukumbi wa Diamond
Jubilee jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Balozi wa Marekani Nchini Dkt.
Inmi Patterson (kushoto) akimkabidhi hundi ya shilingi milioni mbili za
Kitanzania Bi. Rehema Said mshindi wa Tuzo ya I CAN ya Mafanikio katika
Michezo iliyotolewa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Persons with
Disabilities Foundation katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es
Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsalimia Bi.Wakonta
Kakunda (kulia) ambaye ni Mshindi wa Tuzo ya I CAN ya Mafanikio katika
Ujuzi wa Kipekee kwenye hafla ilioandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald
Mengi Persons with Disabilities Foundation katika ukumbi wa Diamond
Jubilee jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu
Katibu Mkuu wa sheria na Katiba Bw, Amon Mpanju katika hafla ya Tuzo ya
I CAN ya heshima inayoandaliwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Dkt.
Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation iliyotolewa leo
katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya I CAN ya
heshima kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
John Pombe Magufuli kutoka kwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Dkt. Reginald
Mengi Persons with Disabilities Foundation Dkt. Reginald Mengi (kushoto)
kwa kutambua mchango wake katika kusaidia watu wenye ulemavu. (Picha na
Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wageni waalikwa
kwenye Tuzo ya I CAN inayoandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi
Persons with Disabilities Foundation Dkt. Reginald Mengi.
Sehemu ya
Watu wenye Ulemavu waliohudhuria hafla ya utoaji tuza ya I CAN pamoja
na chakula cha mchana iliyoandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi
Persons with Disabilities Foundation katika ukumbi wa Diamond Jubilee
jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
………………………………………………………………………………….
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewahimiza watu wenye
ulemavu kutumia fursa zilizopo katika kujikwamua kiuchumi.
Makamu wa Rais ameyasema hayo
leo kwenye hafla ya utoaji tuzo ya I CAN kwa watu wenye ulemavu
iliyoandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Foundation, iliyofanyika
leo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.
“Serikali
inapenda kuwahakikishia kuwa changamoto za walemavu zinafanyiwa kazi
moja baada ya nyingine.”Alisema Makmu wa Rais. Aidha, Serikali
imeendelea
kuweka mifumo, taasisi mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu kwa
kuhakikisha kuwa kuna miundombinu wezeshi ya elimu, afya na teknolojia
ili watu wenye ulemavu kuajirika kwenye viwanda vyetu. “Nitoe rai kwa
waajiri na
wamiliki wa viwanda kote nchini kuhakikisha kuwa hawabagui wala
kunyanyapaa walemavu katika kuijenga Tanzania ya Viwanda ambayo ni
jumuishi kwa wote” alisisitiza Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais amesema Serikali
inatambua, inathamini na inapongeza jitihada za Dkt. Reginald Mengi
pamoja na taasisi yake mpya ya Dkt. Reginald Mengi Persons with
Disabilities Foundation ambayo pamoja na mambo mengine inahimiza
ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu katika ajira.
Vilevile Makamu wa Rais
aliwaambia wananchi waliohudhuria hafla hiyo kuwa Serikali imeweka mkazo
maalum katika masuala ya elimu jumuishi ambapo watu wenye ulemavu
watasoma vizuri kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari.
Kwa Upande mwingine Naibu Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Watu Wenye
Ulemavu Mhe. Stella Ikupa amesema Tuzo za I CAN zimekuwa chachu sana kwa
watu wenye ulemavu ambapo alimpongeza na kumshukuru Dkt. Reginald Mengi
kwa moyo wake wa kipekee wa kutambua na kuwasaidia walemavu.
Aidha, amesema Serikali ina
mpango endelevu wa kutoa elimu ya masuala ya ulemavu ikiwa pamoja na
kuendelea kufanya jitihada za kuongeza wakalimani wa lugha za alama. Kwa upande wake Naibu Katibu
Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa James Mdoe amesema
sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 inatambua fursa na haki sawa
katika kupata elimu hivyo Serikali inaendelea kuboresha miundombinu
wezeshi kwa wote wenye mahitaji maalumu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...