MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga NHIF umejipanga kuhakikisha
inatoa elimu ya kutosha kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kujiunga na Bima
ya afya iliyoboreshwa .
Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Mfuko huo Mkoani Tanga, Ally
Mwakababu wakati akizungumza na MTANDAO huu kuhusu walivyojipanga
kuhakikisha wanaongeza wananchi na kuboresha huduma zao.
Alisema kuwa iwapo wananchi wataweza kupata uwelewa wa kutosha kuhusu
umuhimu wa kuwa na kinga ya matibabu kabla ya kuugua wataweza kuwakomboa
wananchi wengi.
“Hakuna mtu au kiongozi ambaye atakuwa tayari kuongoza wananchi ambao ni
goigoi wa maradhi hivyo Bima ya afya tumejipanga kuhakikisha kwanza
tunaongeza idadi ya wanachama lakini kupitia wao tutaweza kuboresha
huduma katika vituo vya afya”alisema Mwakababu.
Hata hivyo Mwakababu alisema kuwa licha ya mkoa wa Tanga kuwa wapili kwa
uandikishaji wa bima ya afya ya jamii CHF lakini bado eneo hilo
hawakuweza kufanya vizuri zaidi hivyo kwa mwaka huu wamejikita katika
kuongeza uhamasishaji zaidi.
Alisema kuwa wamejipanga kufanya hamasa kuanzia ngazi ya mkoa hadi
vijiji kwa kushirikisha viongozi wa kiserikali na kisiasa kwa lengo la
kuhakikisha kila mwananchi ndani ya Tanga anaona umuhimu wa kuwa na kadi
ya Bima.
Vile vile akiongelea kadi ya Bima ya Toto afya Mwakababu alisema kuwa
katika kipindi cha mwaka 2017/18 waliweka lengo la kuandikisha watoto
waliochini ya umri wa miaka 18 ,3000 badala yake waliandikisha 913.
Huku kwa walioko katika ngazi ya sekondari na vyuo ambao wanatumia
huduma ya Toto afya kadi waliweza kuandikisha 1435 kati ya malengo
waliyojiwekea ya kuandikisha wanachama 3000.
“Tatizo kubwa ni mwamko mdogo wa wananchi kuona umuhimu wa kuwa na bima
ya afya wao wanasubiri mpaka ugonjwa uwe mkubwa na
kushindwa gharama
za matibabu lakini kumbe kama wangeweza kujiunga mapema wasiweza kupata
huduma bora”alisema Meneja huyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...