Historia ya mwanamuziki Oliver N’Goma katika muziki haitasahaulika kamwe licha ya kuianga dunia miaka minane iliyopita. Alifariki dunia Juni 07, 2010 kwenye Hospitali ya Omar Bongo, jijini Libreville, Gabon.

Kifo chake kilisababishwa na tatizo la figo yake kushindwa kufanyakazi vizuri, ugonjwa ambao alikuwa akipambana nao kwa takriban miaka miwili ya mwisho ya maisha yake.

Wasifu wake unaeleza kuwa alizaliwa mjini Mayumba, Kusini-Magharibi mwa nchi ya Gabon mwaka wa 1959. N’goma alizaliwa alikuwa vipaji vya kupiga gitaa, kutunga na kuimba nyimbo za muziki wa Afro-Zouk na Reggae.

Alipewa jina la utani la "Noli," Alifahamika sana kwa kibao chake Bane cha mwaka wa 1989, ambacho kilivumishwa sana takriban Afrika nzima.
Maisha ya N'Goma katika muziki yanaelzwa kuwa alivutiwa kimuziki kwa mara ya kwanza na baba yake, mwalimu na mpiga harmoni.
Japokuwa alipata masomo yake ya muziki kwa mara ya kwanza wakati ana umri wa miaka minane, alianza kutumbuiza mbele ya hadhara baada ya kuhamia mjini Libreville kwa ajili ya masomo.

Oliver N’goma wakati akichukua masomo ya uhasibu, alijiunga na kundi la Capo Sound, iliyokuwa ni bendi ya shule, ambapo ndipo alipojifunza namna ya kupiga gitaa.

Kundi hilo lilikuwa likipiga dansi rasmi na mipira, ambapo alijifunza sanaa ya kutumbuiza kwenye jukwaa. N'Goma alikuwa mwanafunzi maskini kabisa, aliyejizatiti zaidi kwenye muziki na sinema badala ya masomo.

Mapenzi yake ya filamu yalimuongoza hadi kufanyakazi na TV ya Gabon, ambayo iliwahi kusafiri nayo hadi nchini Ufaransa mnamo 1988 ambapo alijifunza kuwa mtu wa Kamera. Wakati wakiwa katika majira ya baridi huko Paris, alikuwa tayari amemaliza kazi yake ya muziki alioutunga akiwa Gabon.

N’Goma aliwahi kufanya kazi ya muziki kwa pamoja na Manu Lima, ambaye alikuwa mtayarishaji wa rekodi mashuhuri kwa muziki wa Kiafrika. Lima alivutiwa sana na kazi bwana mdogo, na kushikilia mwongozo wa rekodi ya kwanza ya N'Goma iliyokwenda kwa jina la Barre.

Albamu ilifurahia mafanikio ya tabu kwa mara ya kwanza, hadi hapo kituo cha redio cha Kiafrika ilipoanza kupiga nyimbo zake. Jina la wimbo huo ilipata ushindi na mafanikio mengi huko Afrika, Ufaransa, na Ufaransa na West Indies, ulienda kutamba sana katika maeneo hayo.

N’Goma alifurahia mafanikio hayo yakilinganishwa na mafanikio yalipatikana kwenye albamu za Mario ya T.P.OK Jazz, iliyokuwa ikiongozwa na Franco Luanzao Makiadi au Yeke Yeke wa Mory Kante. Albamu hiyo ilipata kuwa moja kati ya albamu zilizouza sana katika albamu za Kiafrika hadi sasa.

N'Goma alitoa albamu ya pili ya Adia mnamo Desemba 1995. Hata hivyo alifanyakazi tena na Manu Lima. Miaka mitano baadaye, albamu yake ya tatu ya Seva ilitoka. Oliver N’Goma aliwahi kuachia albamu ya Best of Oliver N'Goma, iliyokuwa imejumuisha vibao vikali ilitolewa mnamo mwaka wa 2004.

Baadhi ya nyimbo alizoachia Oliver N’Goma zilikuwa za Jump to navigation, Jump to searc, Alphonsine, Lusa, Adia, Muetse, Julie, Icole na Bane. Zingine ni Felly, Shado, Barre, Sal, Muendu, Betty, na Ng’ebe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...