KAMPUNI ya michezo ya kubashiri ya Premier Bet nchini imetoa zawadi kwa washindi wa Jackpot ya soka iliyofanyika Machi 9 mwaka huu huku washindi wawili  wakijinyakulia vitita vya milioni 42.5 kwa kila mmoja.

Akizungumza na vyombo vya habari Meneja rasilimali watu wa kampuni hiyo Amanda Kombe amesema kuwa jamii imekuwa na uelewa mzuri mara baada ya kuzindua na kuhabarisha umma juu ya promosheni hiyo ya jackpot na kueleza  kuwa katika Jackpot iliyochezeshwa Jumamosi jumla ya shilingi milioni 85 zilikuwa zikishindaniwa na washindi wawili wamepatikana ambao ni Flavian Msigala kutoka Dar es salaam na Robert Daniel kutoka Mpanda ambao kila mmoja amejinyakulia kitita cha shilingi milioni 42 na laki tano.

Amanda amesema kuwa washindi hao waliweza kubashiri kwa usahihi mechi zote 12 na wengine 15 waliweza kubashiri 11  na wengine 52 kubashiri kwa usahihi mechi 10 na hao wote wamebahatika kupata kifuta jasho. Amesema kuwa hiyo ni jackpot ya pili kutoa washindi walibaoshiri kwa usahihi zaidi na ikiwa ni jackpot ya 56 kuchezwa.

Washindi wa Jackpot hiyo wameishukuru Premier Bet nchini kwa kutoa donge hilo ambalo litawasaidia kufanya shughuli za kujiongezea kipato kwao na  taifa kwa ujumla.
 Meneja rasilimali watu wa Kampuni ya  Premier Bet, Amanda Kombe(katikati) akizungumza na waandishi wa habari  wakati wa hafla ya kutoa utoaji wa milioni awadi kwa washindi wa Jackpot ya soka iliyofanyika Machi 9 mwaka huu huku washindi wawili  wakijinyakulia vitita vya milioni 42.5 kwa kila mmoja leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja Masoko wa  kampuni ya  Premier Bet, Benjamin Mnali.
 Meneja Masoko wa  kampuni ya  Premier Bet, Benjamin Mnali akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mchezo wa kubahatisha pamoja na namna ya kujiunga kwenye michezo ya kampuni hiyo wakati wa hafla ya kutoa utoaji wa milioni awadi kwa washindi wa Jackpot ya soka iliyofanyika Machi 9 mwaka huu. Kulia ni Meneja rasilimali watu wa kampuni ya  Premier Bet, Amanda Kombe
 Mshindi wa Jackpot ya soka, Flavian Msigala kutoka Dar es Salaam akizungumza na waandishi bara baada ya kukabidhiwa kitita cha shilingi milioni 42 na laki tano leo jijini Dares Salaam.
 Mshindi wa Jackpot ya soka, Robert Daniel kutoka Mpanda akizungumza na waandishi bara baada ya kukabidhiwa kitita cha shilingi milioni 42 na laki tano leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...