Kufuatia kusuasua kuanza kwa miradi ya kimkakati, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amewaagiza Wakuu wa Wilaya za Ilala na Kinondoni, Wakurugenzi wa manispaa na wakuu wa idara kuhakikisha hadi kufikia Jumanne ya March 26 miradi yote iwe imeanza utekelezaji ikimaanisha kuwa mikataba imesainiwa na mkandarasi yupo kazini.

RC Makonda amefikia hatua hiyo baada ya kuchukizwa kuona miradi haijaanza kutekelezwa hadi sasa licha ya Rais Dkt. John Magufuli kutoa fedha zote za miradi lakini baadhi ya watendaji wamekuwa wakichelewesha kuanza kwa miradi.

Aidha RC Makonda amempa Siku tatu Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bi. Sophia Mjema na Mkurugenzi wa manispaa hiyo kuhakikisha mkataba wa ujenzi wa machinjio ya kisasa Vingunguti unasainiwa mara moja na mkandarasi anaanza kazi.

Hivyohivyo RC Makonda amempa siku tano Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni na Mkurugenzi wake kuhakikisha ujenzi na Maboresho ya ufukwe wa kisasa wa Coco unaanza mara moja.

Mhe. Makonda amesema endapo wahusika watashindwa kutekeleza agizo hilo watatafsiriwa kuwa wameshindwa kusimamia fedha na miradi ya serikali.

Itakumbukwa mwaka jana Rais Dkt.John Magufuli alitoa fedha za kutosha kwaajili ya miradi ya kimkakati ya kuwakwamua wananchi ikiwemo ujenzi wa barabara, hospital, zahanati,vituo vya daladala,maji,umeme,elimu na machinjio ili kupunguza kero za wananchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...