Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakitoka kukagua jengo la masijala ya ardhi kijiji cha Mbondo wilayani Nachingwea linalojengwa kupitia MKURABITA wakati wa ziara ya kamati hiyo yenye lengo la kukagua miradi ya maendeleo mkoani Lindi.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Jason Rweikiza (Mb) akieleza umuhimu wa hatimiliki za kimila kabla ya kuwapatia wananchini wa kijiji cha Mbondo wilayani Nachingwea wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani Lindi.
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mwanne Mchemba (Mb) akitoa wito kwa wananchi wa kijiji cha Mbondo wilayani Nachingwea kuchangamkia fursa ya hatimiliki za kimila wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani Lindi.
 Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akieleza azma ya serikali ya kuwainua wanyonge kwa kuwapatia hatimiliki za kimila ili waweze kujikwamua kiuchumi.
 Wananchi wa kijiji cha Mbondo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Jason Rweikiza (Mb) alipokuwa akizungumza nao juu ya umuhimu wa hatimiliki za kimila wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani Lindi.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, MJason Rweikiza (Mb) akitoa hatimiliki za kimila kwa mmoja wa wananchi wa kijiji cha Mbondo wilayani Nachingwea wakati wa ziara ya kamati yake ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani Lindi.
Mtendaji Mkuu wa MKURABITA, Seraphia Mgembe akizungumzia umuhimu wa wananchi wa kijiji cha Mbondo wilayani Nachingwea kumiliki hatimiliki za kimila wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa yenye lengo la kukagua miradi ya maendeleo mkoani Lindi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...