Dar es Salaam. Shabiki wa Simba na mkazi wa mkoa wa Songwe, Willy Mwakapembe Wadson ameshinda Sh 123,614,160 baada ya kubashiriki kwa usahihi jumla ya mechi 12 katika za  mchezo wa kubahatisha wa Perfect 12 unaondeshwa na kampuni ya M-Bet Tanzania.
Mwakapembe ambaye ni mfanyabiashara ndogondogo na mkulima wa Tunduma anakuwa mshindi wa tatu tokea kuanza  mwaka huu  kushinda kiasi kikubwa cha fedha ambacho amesema kitabadili maisha yake.
Washindi wengine ni Frank Kayombo  ambaye alishinda kiasi cha Sh milioni 188.4 wakati mshindi wa pili alikuwa Simon Muray aliyeshinda Sh milioni  81.
Meneja Masoko wa M-Bet, Allen  Mushi pia alisema kuwa kuna washindi wengi waliojishindia mamilioni kupitia Jackpot Bonus ya kampuni yao.
Mushi amesema kampuni yao inazidi kupata washindi na mpaka sasa jumla ya Sh milioni 500 zimetumika kuwazawadia washindi mbalimbali.
Alisema kuwa kampuni yao inazidi kuwabadili maisha Watanzania huku wakichangia pato la serikali kiasi cha Sh milioni 24.7. Alisema ili kuweza kucheza bahati nafasi hiyo unaweza kutembelea http://bit.ly/2VZCB38 ili kuanza kuanza kubet.
“M-Bet inazidi kuchanja mbuga na kuinua vipato vya Watanzania na kuchangia maendeleo ya nchi chini ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Dk John Pombe Joseph Magufuli. Nawaomba Watanzania kucheza  ili kushinda zawadi za fedha,” alisema Mushi.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha zake, Wadson alisema kuwa alianza kubeti muda mrefu kabla ya kupata ushindi huo mnono.
Alisema kuwa hakukata tamaa pamoja na kutaniwa na marafiki zake wengi kuwa hataweza kushinda fedha nyingi zaidi ya kupoteza muda wake.
“Sikukata tamaa na kuendelea kubeti, niliamini kuwa siku moja nitapata bahati ya kushinda, nashukuru Mungu kupata kiasi hiki cha fedha na nitakaa mke wangu kupanga jinsi gani ya kuwekeza na kujiongezea kipato,” alisema Mwakapembe.
Meneja Masoko wa Kampuni ya M-Bet Tanzania, Allen Mushi (Kulia) akikabidhi mfano wa hundi, Willy Mwakapemba  (katikati) kutoka mkoa wa Songwe aliyeshinda Sh Milioni 123.7 za mchezo wa Perfect 12 wa kampuni ya M-Bet Tanzania. Anayeshuhudia ni  Kaimu Msimamizi wa Kitengo cha Michezo ya Kubahatisha, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi, Ilala Philipo Haule. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...